MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

mgonjabc1

Kama ulidhani ya mwaka 2008 ndio yashaisha basi ulikosea.Mambo yangali yakiendelea.Katibu Mkuu wa zamani wa Wizara ya Fedha na Mipango,Bw.Gray Mgonja leo ametinga kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Henzron Mwankenja, akikabiliwa na mashtaka mbalimbali.Mojawapo ya mashtaka anayokabiliwa nayo ni pamoja na matumizi mabaya ya madaraka kama ilivyokuwa kwa mawaziri wa zamani wa wizara hiyo nyeti, Daniel Yona na Basil Mramba waliofikishwa kizimbani wiki mbili zilizopita.

Habari hii inaendelea…stay tuned.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

48 Responses to “NI ZAMU YA GRAY MGONJA!”

  1. Comment by kekuuu on December 15th, 2008 10:57 am

    yaani wewe wasikupe hata dhamana….nenda tu moja kwa moja ukanyee dembe

  2. Comment by C16 on December 15th, 2008 11:03 am

    Wamfunge huyo

  3. Comment by eve on December 15th, 2008 11:24 am

    haya sasa twende kaziiiiiiiiiii sangulo ohhhh!!!! sangulo mamaaaaaaaaaaaaa oh sangulo ohhhhhhh sangulo mamaa!!!!!!! huyu hata mimi nasapoti asilimia mia lakini si mramba aende bwanaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!! habari ndo hiyo xmass selo akikakaaaaaaaaaa!!!!!!! hey mgonja weka w tumalizane mgonjwaaaaaaaaa wa segerea matanuzi kwishaaaaaaa kazi na kale kademu kako kanakojidai sijui itakuwaje heheeheeeeeeeeeeeeeeee!!!!!!!!

  4. Comment by emergencypoison on December 15th, 2008 11:52 am

    hahaha…wewe eve umenichekesha mpaka nimetaka kufa hapa kitini… naona umeanza kula sanguloo….we mkali…now let them face the music. washenzi sana hawa culprits.

  5. Comment by Mwanamke wa shoka (UK) on December 15th, 2008 11:52 am

    mhhh!!…I hope this is not another “Changa la macho”, lol

  6. Comment by Mwanamke wa shoka (UK) on December 15th, 2008 11:55 am

    Gets into mi nevu nao…..it is so theatrical…..that I just cant stop worrying….

  7. Comment by Oxalato on December 15th, 2008 11:04 am

    Nshafungulia nyuki usitoke nduki,weka kigingi niweke chuma,weka mafisadi niweke mahakama ya kisutu…hapa vumbi tuuuu na wengine wanakuja….na baaado

  8. Comment by hombiz on December 15th, 2008 11:05 am

    Bandika mandua ndo mchezo unaotakiwa ktk hii draft!
    JK, “hata kama kete ni za moto”, endelea kuzisukuma hadi tuingie king!. Ila tusitoke bila bila!…a.K.a Changa la macho “kama baadhi ya wana BC Blog wanavyotabili

  9. Comment by Lalola on December 15th, 2008 11:08 am

    We Eve wewe, jamani umenichekesha mno. duh hadi nimeshikwa na kwikwi kwa kuchek. Kama wacheza Sangulo mi naongezea Ndombolo ya Solo…….

  10. Comment by ROss on December 15th, 2008 11:56 am

    Acheni chuki binafsi

  11. Comment by Frateline on December 15th, 2008 12:45 pm

    Hi guys

    Kwa kweli Jk ameamua kuwapa meno PCB pamoja na DPP sasa kazi tunaiona hawa watu wamelihujumu sana taifa, sasa za mwizi ni arobaini,

    Mimi siamini kama ni changa la macho kwa kuwa hawa wanao kamatwa ndiyo vigogo wenyewe ambao wamekaa wizara ya fedha miaka nenda miaka rudi- Kwanza aibu yenyewe ni tosha-character assasination hawa jamaa ni kwisha kisiasa na hata kesi zao zikichukua muda mrefu lakini aibu hii itawaua kwa pressure maana hawa jamaa wanapesa chafu, ndiyo mana Chenge alisema zake ni vijesenti- mwendo uwe huo huo JK

    Frateline

  12. Comment by dan on December 15th, 2008 1:10 pm

    we Ross Hawala yako nini?
    Jk, Thumb up!!!!!!!!!!!! Endeleza makamuzi, mafisadi wote mpaka waishie Segerea! Nina Machungu sana na Tz yangu! Inanuma mno kuona rasilimali tulizopewa na Mwenyezi zinaishia kwenye mikono ya watu wachache tu kama kama akina Mgonja. Kamata pia Mkapa! weka selo! maana yeye ndiyo alikuwa anawakingia kifua!

  13. Comment by binti-mzuri on December 15th, 2008 1:27 pm

    lol @ sangulo.. sijausikia long time..ila mbona comments zingine hazielewekii mara zije kabla,mara baada…mmmh..anyways.. hili nalo changa la macho?i stick to what i said before..sidhani kama ni changa la macho..tanzania yes we can..

    btw jeff,hongera..naona kuna ki button cha notify follow-up comments au sijui mi ndo mshamba sijaja long time.hakijaharibika kitu

  14. Comment by mdau on December 15th, 2008 2:58 pm

    Wadau naona sasa ngoma inogile……….

  15. Comment by Mwanamke wa shoka (UK) on December 15th, 2008 4:52 pm

    mdahalo upo wazi, lol…..(*0)

  16. Comment by BLACKMANNEN on December 15th, 2008 11:06 pm

    Wahenga wanamsemo usemao “Mchumia Juani, Hulia Kivulini”. Lakini Watanzania wa karne ya JK tunasema “Mchumia Kivulini, Hulia Juani”. Ni lupango tu wote.

    Tena Segerea ndiyo ilikuwa inawafaa sana ninyi mlionona kama ulivyo wewe Mgonja na wenzako akina Yona na Mramba. Mramba bado hajakoma, ukimtazama usoni mwake. Halafu Mramba ana “ngebe” kweli kweli kwa wanahabari.

    Blackmannen

  17. Comment by Weezy on December 16th, 2008 12:01 am

    Mafisadi WANYONGWE!

  18. Comment by Trojen on December 16th, 2008 12:56 am

    Mi ningekuwa wewe JK, hata dhamana nisingewapa hawa, kwani hawakujua, si tunakula majani, wao na V8 za kisasa, na majumba mazuri tuu. Pia ifanyike uchunguzi ikigundulika kifungo maisha na kuwafilisi wote mzeiya!

  19. Comment by SaLaMA on December 16th, 2008 1:36 am

    hahahahahhahahhahhahhahahhahhahahhahahhaaaaaaa EVE UMENIFANYA NIMECHEKA KWA SAUTI WEWE HEHEHEHEHEHE UWIIIIIIIIIIIIIIIIIIII KADEMU KAKE KANAJIDAI.

    ILA JAMANI MIE KUKAMATWA KWA HAWA MAFISADI NAONA NI KITU KIDOGO SANA NACHOSUBIRI MIMI KAMA MIMI HUKUMU TU ITAKUWAJE?

  20. Comment by mwanaharakati on December 16th, 2008 1:48 am

    vizuri saaana uliona kituibia hela zetu raha sana, sasa naukome, wewe ni kibaka kama vibaka wengine. Nbado ho wenzako wote watafutwe, nawapelekwe kunako husika, Raisi ukiwafumbia macho vibaka wengine wa serikali hii, hapa hapatakalika, wezi ni wezi tuu, wamanzese fungwe wa serikali anyongwe kabisa.

  21. Comment by halima on December 16th, 2008 2:00 am

    Hivi nyinyi mnaong’ang’ania changa la macho mnamatatizo gani? au mnataka akamatwe nani ndio mridhike? ovyoooooo

  22. Comment by george on December 16th, 2008 2:04 am

    aende tu jela huyo,ameshakula sana bila hata ya kuwahurumia wa tz wanaopata tabu.

  23. Comment by Mattylda on December 16th, 2008 2:11 am

    Safi sana JK! Mgonja utakula x-mas na babu seya mpe company na wanae huko wasiboreke!!!halafu bado yule rafiki yako mnao kutanaga vikao vya usiku kwenye lager nyooooo!!

    Eve na wewe nae kiumbe shosti sanguloooooooooooooo oooooo aiiiii na wewe Lalola inakuwaje shostito??naona maoni ya eve umeyaona before au ndo ni aje??mbona sielewi hapa???

    ROSS MTOTO WA FISADI a.k.a MTOTO MSHUA WA MASAKI unasema??eti chuki binasfi- unamjua vizuri huyu baba pichani au unaongea nini???hebu tupe nafasi hapa LOL!

  24. Comment by Sakina on December 16th, 2008 2:59 am

    Duh!huyu Fisadi haswa numbari one mke na watoto hawajawahi ishi TZ wako USA na mke alikuwa anatamba hawezi beba mabox mume kila end of the month 20,000 USD anamtumia duh!huyu JK weka msumari wa moto aitoke tena dhama 10 billions cash!

  25. Comment by Fukara on December 16th, 2008 3:15 am

    ah sasa yametimia huyu ndo alikuwa connector
    anameremeta

  26. Comment by Maisha on December 16th, 2008 3:42 am

    Its time for them to fill the pinch for what they did for our nation, kwa sababu tu walikuwa na mamlaka wakasahau kama na wao wako chini ya sheria.

  27. Comment by mukaru ng'ang'a on December 16th, 2008 3:51 am

    Wizi Mtupuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu

    Wizi mtupuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu

    Bado Chenge,Karamagi,Masha,Lowasa,Makamba,Malima na Jakaya Mrisho Kikwete

  28. Comment by hombiz on December 16th, 2008 10:54 am
  29. Comment by ndalo on December 16th, 2008 11:22 am

    Huyu jamaa inasemekana aliwanyima kibari cha msamaha wa
    kodi ya bandari wazee wa kukaanga mbuyu,walipotaka kupeleka vifaa vyao vya mziki bongo,nao wakamkaangia mbuyu

  30. Comment by Lalola on December 16th, 2008 11:24 am

    Mwenzangu Mattylda hata mie nashangaa, coz maoni ya Eve nliyaona hapo juu ndo na mie nikaandika comments zangu. Makubwa haya, au wanataka kutufisadi na sie wanaBC????

    Mhhh, langu jicho.

  31. Comment by papuu on December 16th, 2008 1:54 pm

    tunaweza kuongea kwa facts kidogo kama wewe mukaru ng’ang’a unayetaka jakaya mrisho kikwete akamatwe kwa kosa lipi hasa yusuf makamba kafanyeje yani listi yako ya kichwara nyie ndio pampula mnaodandia mada hapo hata taarifa za habari husikilizagi basi umeacha kuwataja mafisadi BENJAMIN WILLIAM MKAPA na ZAKHIA MEGHJI unataja watu ambao hawajafanya lolote baya bila kumsahau lowasa,nashangaa mpaka sasa hajafikishwa kizimbani kujibu mashtaka hili changa la macho mazee kama la hapo juu la huyo lalola

  32. Comment by Mwanamke wa shoka (UK) on December 16th, 2008 2:37 pm

    miye nasubiria tuu kusikia wapepata miaka kadhaa ama mufilisi…..pungufu ya hapo ni changa la macho mweee..!!!!!!!!

    …nimekula chumvi…… naelewa kata funua za kabumbu…..lol…..

  33. Comment by Mattylda on December 17th, 2008 1:26 am

    Lalola mhh hapo pana utata kidogo anyway tutafika!!!!!!!!!!

    Jamani msaada tutani kwani Edwin Ndaki kapotelea wapi siku hizi?????

  34. Comment by eve on December 17th, 2008 1:56 am

    hahahahahaa huwa nashindwa kuelewa nikituma comment inatake long time kuaccept inakuwa kwenye moderation changa la macho hilo mie sielewi wadau

  35. Comment by kevin on December 17th, 2008 4:06 am

    sasa kidonda kimetiwa pilipili chumvi na malimao ya kutosha..kama ni upande wa msosi bado saaaaana..tushapewa chipsi mayai na tomato mmmmh tell me kimemis nini?ok tuseme wote chumvi,chill na chachanduuuuuuuuu…ndo tunachotaka kipara,mvi kile kiti kidogo cha kukalia jikoni,na wengine waende jela wakapigwe mashine.

  36. Comment by Mwanamke wa shoka (UK) on December 17th, 2008 12:32 pm

    teh teh teh…..mdahalo naona umenoga….yep

    Niwatakie Xmas yenye kujaa furaha tele na mwaka mpya wa 2009 uliosheheni mafanikio na afya tele….ndio umefika huo….2010 nao haupo mbali…..lol

  37. Comment by BLACKMANNEN on December 18th, 2008 3:57 am

    BC Editors,

    Maoni yetu mbona yanawangoja karibu siku nzima ili kuyachapisha? Au mnasubiri watu wengi waandike ndipo mchapishe?

    Blackmannen

  38. Comment by Mwanamke wa shoka (UK) on December 18th, 2008 1:54 pm

    mhhh sio siri…naona ma-editors wapo X-mas holidays already……sio mbaya …..early birds….

  39. Comment by binti-mzuri on December 18th, 2008 2:10 pm

    haha kevin mie hoi ka kucheka

  40. Comment by Dunda Golden on December 19th, 2008 2:04 pm

    KAZI BADO KUBWA LAKINI TUMEBAKI HATUJUI WAPI TUNAKWENDA INGAWA NI WACHACHE WANAOJUA TULIPOTOKA
    AIDHA KWA LOLOTE

  41. Comment by mdau on December 19th, 2008 4:11 pm

    Kikwete kanyaga moto twende baba,Usiangalie tuta wala shimo.Ni mwendo mdundo tu tu Brother Jakaya.

  42. Comment by papuu on December 20th, 2008 5:44 pm

    kashatolewa kwa dhamana

  43. Comment by BLACKMANNEN on December 21st, 2008 2:29 am

    Wewe “papuu”,

    Alipotolewa Mgonja, wewe ulijisikiaje? Ulijisikia raha ama maudhi?

    Blackmannen

  44. Comment by papuu on December 21st, 2008 8:40 pm

    wewe ‘blackman’

    at this point i dont think it matters mimi nilijisikia furaha au maudhi kwani jamaa anadunda mtaani na mokasin yake ya guchi.sasa sijui nikusahidiaje hapo?

  45. Comment by j4 on December 22nd, 2008 5:03 am

    halloooooooooooooooooooooooooooooooo,, huyu FISI YAADI
    anapaswa asome those coments ili ajuwe kwamba wa TZ wamemchoka hata akidondoka chini akuna wakumlokota,

  46. Comment by so upset on December 22nd, 2008 3:38 pm

    mgonja fisadi,hela za zamana kazitolea wapi kama sio ufisadi huu.afungwe jela maisha

  47. Comment by Global Voices Online » Tanzania: Fight against corruption intensifies on December 23rd, 2008 5:34 pm

    [...] about to be taken to court that morning on allegations of abuse of office. And Bongo Celebrity [Sw] confirmed later on that indeed Mr. Mgonja had appeared in court. Praising the president one reader wrote: JK [...]

  48. Comment by BLACKMANNEN on December 28th, 2008 4:25 pm

    Gray Mgonja, umshukuru Mungu kuwa Tanzania. Pia shukuru Jakaya Kikwete, ni Rais anayetawala kwa kufuata Utawala wa Sheria.

    Gray Mgonja, kama ungekuwa ni mGuinea, kwa Captain Musa Kamara, Kiongozi mpya wa nchi hiyo. Ungenyongwa na wenzako wote, bila ya kufikishwa Mahakamani.

    Kiongozi mpya wa Guinea, ametangaza kuwa, atapitia upya mikataba yote ya uchimbaji madini ya nchi hiyo. Kama atagundua kuwa, kulikuwa na rushwa au ubadhirifu wowote katika mikataba hiyo, atawakamata wote wanaohusika na UFISADI huo na kuwanyonga, bila ya kuwafikisha Mahakamani.

    Guinea-Conakry, ni nchi tajiri yenye madini kibao, lakini wananchi wake ni maskini wa kutupwa. Baada ya kufa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Lamizana Conte. Captain Camara, amechukua Utawala wa nchi ya Guinea kwa nguvu, ili kukomesha rushwa iliyokidhiri serikalini, na katika mashirika ya umma. Habari ndiyo hiyo!

    This Is Black=Blackmannen

Leave a Reply