MY TANZANIA   |   PLACES TO GO   |   MEDIA   |   ONLINE ENTERTAINMENT    

Kwa mila na taratibu za jamii nyingi,hususani zetu za kiafrika,kijana akifikia umri fulani huwa anategemewa kuoa.Ikitokea ukafikia umri ambao kila mwanajamii anakutegemea “kujipatia jiko” na ukawa hujafanya hivyo, hapo lazima ujiandae na swali;unaoa lini?Ukikutana na shangazi swali ni hilo hilo.Ukikutana na mjomba naye anasimamia hilo hilo.Jamii nzima inauliza,unaoa lini?

Sasa je ukiulizwa swali hilo huwa unajibu nini?Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya,Hamis Mwinjuma a.k.a MwanaFA a.k.a Binamu anakupa msaada wa majibu katika single yako mpya inayokwenda kwa jina Bado Nipo Nipo huku akiwa amemshirikisha Miss Universe Tanzania 2007,Flaviana Matata.

Bado Nipo Nipo imepikwa na producer Harmy B.Pia MwanaFA anapewa tough na vichwa vingine kama vile Ambwene Yesaya(AY),Alan,Jabiri,Shehe na mwanadada aitwaye Anna.

Usikilize wimbo Bado Nipo Nipo kwa kubonyeza player hapo chini.Ningependa sana kusikia majibu kutoka kwa kinadada walio single, ni kweli anayoyasema MwanaFA?

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Share and Enjoy:
  • Digg
  • Sphinn
  • del.icio.us
  • Facebook
  • Mixx
  • Google Bookmarks
  • email
  • LinkedIn
  • Live
  • Spurl
  • Technorati
  • Yahoo! Buzz
  • YahooMyWeb

Feedback / Comments

42 Responses to “MwanaFA UNAOA LINI…?”

  1. Comment by pandu on July 1st, 2008 2:25 am

    Bado nipo nipo mama…..ukiitwa boyfriend usidhani upo peke yako, sura za utoto lkn wanaifadhi wazee wako, sijui ni tamaa, dhiki au wanaanika njaa tu
    Ukimegemwa dem wako nawe mtafute mnyonge ummegee, aipunguzi maumivu ila inadhihilisha ukidume.
    FA ni nyoko mwana…nimekukubali

  2. Comment by P. S. Nalitolela on July 1st, 2008 2:39 am

    nimesikiliza an uncorrupted version from binamu13.com, and I must say, it’s like Binamu is talking to me!! Totally feel what he’s saying, nimeikubali!!

  3. Comment by H. Dignified. on July 1st, 2008 4:54 am

    Hii ngoma nimeikubali. Ni bonge la song na linatisha si uongo. Mzee uko juu sana tu. Ata “mimi bado nipo nipo kwanza”. Na mademu wenyewe hawa wa siku hizi yaani “Nipo nipo sana tu”.

  4. Comment by neema on July 1st, 2008 10:26 am

    upo juuu mwana

  5. Comment by hans on July 1st, 2008 10:49 am

    eeh bwana unatisha si utani, wewe ni mzee wa vina kila unachosema ni kweli tupu. hii hata wakisikia ndugu zangu wanaonikomalia nioe wenyewe watazima story. asante sana BINAMU F.A

  6. Comment by DUNDA GALDEN on July 1st, 2008 11:53 am

    Bado niko niko kwanza…….
    alilala na bibi harusi wakati si bwana harusi
    nimeupenda huu ujumbe lakin si kwa wanawake wazuri
    msela yeye ndio wazo lake poa mwana uchune ipo siku
    uakutana na mabinti wazuri hapo utachagua kama mimi
    msela wako nilivyochagua baada ya NIPO NIPO YA KIPINDI
    KILICHOPITA
    Chai goda

  7. Comment by hombiz on July 1st, 2008 2:36 pm

    vicheche wengi sana siku hizi. Sio BONGO tu hata nchi za watu wapo. Cha muhimu ni kumuomba mungu akusaidie kupata mwanamke anayekufaa. La sivyo utazeeka bila kuoa.

  8. Comment by baker on July 1st, 2008 3:53 pm

    Ebwana FA nimekubali yani toka nianze kusikiliza music wa bongo, ndio leo nasikia hii tune yako na ninavyoona ndio nyimbo ambayo iko na full maujumbe yaliko kwenye maisha yetu haya ya kiswahili. Ebwana FA umelenga kamanda yani pale pale,penyewe mwana. Duh ebwana I cant wait to get ur album men! its cracking tune.Big up

  9. Comment by echo on July 2nd, 2008 6:38 am

    ebwana dah! nimekukubali mkubwa uko juu ile mbaya katika tungo, nyimbo yako nimeikubali sana iko inaendana na hali jinsi ilivyo sasa…..! wimbo umenigusa sana kwani wazo hilo lipo kichwani mwangu muda mrefu sana nanihawahi kumjibu binti mmoja hvyo hyo kutokana na swali kama hilo…..nlidhani niko peke yangu kumbe tuko kibaaaaoooooooooooooo! BADO NIPO NIPO TU, SAAAAAAAANA TU!!!?

  10. Comment by dadi on July 2nd, 2008 6:55 am

    Ndio mkubwa uko juu si kitoto nyimbo nzuri ujumbe bab kubwa………….! mtindo wa sasa ni kumegana tu hakuna mapenzi, ni kama mchezo flani hivi inatakiwa full maujanja uongo c kpole pole…….! hakuna ndoa, ukioa umeolea watu kuna vijamaa flani dem mzuri kwao mpaka awe wa mtu. mabint tamaa zimewazidi. bado nipo nipo tu sana tu, wakuoa ntakuwa mimi, nioe unimegee! Ayaaaaaaaaaaaaaah weeeeeeeeeeeeeeeeee!!!!!? big up fa.

  11. Comment by mzee wa vichanchubi on July 2nd, 2008 8:59 am

    uko juu mwana ila achana na visungura tope,bado nasubiri cd yangu mwana,misijabisha!!!!!!!!!!Big up

  12. Comment by binti-mzuri on July 2nd, 2008 3:36 pm

    mh we hombiz nawe…mnaonaga wanawake tu…mbona wanaume hawasemwi!?!?who wants to get married to a player!?NOT ME

  13. Comment by karen on July 3rd, 2008 1:00 am

    Kaka wimbo mzuri sana big up,
    ila kwa nyinyi wasanii ndio mnapenda wanawake wa hi class ndio maana mnakutana na matatizo,jaribu kukaa uchunguze wasani wenzako woote yupi anamsichana wa low class?
    na wanawake wa sikuizi jamani tupendane,manake wanawake nao wamekuwa maadui hata mugabe anaafadhali
    hawajui huyu mume wa mtu au huyu lover wa rafiki yangu hasa hawa wanojiita wasomi,

    tuwe makini la sivyo tutaisha na hiv jamani

  14. Comment by Jafa on July 3rd, 2008 7:29 am

    binti mzuri..
    naona MwanaFA has made a big point hapa,ila anaongelea upande wake kama mwanamme…lakini it applies for both!…namjua mtu alikuwa anaoa jumamosi na akalala kwa sunguratope mmoja hivi Friday…mtu maarufu tena

  15. Comment by sally on July 3rd, 2008 8:17 am

    Big up

  16. Comment by binti-mzuri on July 3rd, 2008 1:46 pm

    oke poa jafa! ila mbona unaonesha kushangazwa!?!?..ndio maisha!…’nipe nikupe,raha tupateee’

  17. Comment by iAUWDQ on July 3rd, 2008 9:14 pm

    Huwa simkubali MwanaFA ila sasa nime mkubali maana ule mwimbo wa “Unaoa lini ” yaani yale majibu najiona kama nimeandika mimi ,maana kila kitu ni kama ninacho jibu nikiulizwa swali hilo.

  18. Comment by Miss G on July 4th, 2008 5:58 am

    Wewe nae unataka kushangaza uma kwamba huwa humkubali mwana FA, basi unaonekana kichwa chako kigumu kweli, he hehehe
    Big up sana Mwana FA, wimbo umesimama sana kama kawaida yako….hata sisi mabinti bado tupo tupo!!! mapenzi yenyewe haya ya kibongo bongo! umenena ukweli mtupu

  19. Comment by mr b on July 4th, 2008 9:32 pm

    imenibidi niucjilize huu wimbo baada ya kusoma comments zenu..wimbo ni mkali na binamu huwa hakosei ila tuangalie tusijidanganye coz excuse huwa haziishi…unayosema binamu ni kweli yapo ila tiba sio kuwepowepo..hivi kweli ukitaka kwenda kwenu tanga utasubiri madereva walevi na wavunja sheria za bara2 waishe,hali ya hewa iwe safi ndo usafiri ili usipate ajali? hope jibu unalo,wat u’l do is 2 take precaution nakuanza safari…afterall huwezi kueliminate all problems ndo uoe,uwezo wa mwelevu huonekana kwenye kutatua tatizo litokeapo na si kumbia kwa kuliogopa….young man peter s.n acha kujifaliji oaaaaaaaaaaaaaa……………..

  20. Comment by ALBERT MBAGO on July 5th, 2008 6:14 am

    Ebwana big up sana BINAMU, track imetulia kinoma umeongea ukweli kuhusu hawa dada zetu, mi mwenyewe bado nipo nipo kwanza tena bado nipo nipo sana, maana life lenyewe limepinda sana bado upate mwanamke wa simu na gari au mkwanja na gari si utakojoa dagaa mwanaume. Bado nipo nipo sanaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

  21. Comment by Frateline on July 7th, 2008 11:57 am

    Hi guys, Mimi kutoka Helsinki- Finland
    Kwa kweli song ni zuri, Lakini wasi wasi wangu huu wimbo umekaa upande mmoja wa shilingi, halafu kwa watu wasio makini unapotosha maana umewaweka wanawake kwenye kundi moja, It is too general, kwani ndiyo wapo wanawake wenye sifa mbaya lakini pia wapo wanawake wenye sifa nzuri ni wengi tu, vivyo hivyo hata sisi wanaumme tupo ambao tabia zetu chafu sana yaani umalaya wa ajabu, na mara nyingi wanaumme wengi ni malaya muno, wengine walevi sana na hawana sifa za kuwa waumme za watu, hivyo sio vizuri kuwanyoshea vidole mabinti wakati wewe mwenyewe na mungu wako unajua ni malaya wa kutupwa, biblia inasema nitakupa wa kufanana naye, wewe malaya halafu unataka bikira itoke wapi, wakati wewe ni mchafuzi na unaharibu mabinti wa watu. Kwanza wanaume wengi wanapenda kudanganya mabinti wa watu kuwa nitakuoa na baada ya kumega anaingia mitini, kwa kweli dada zetu wakati mwingine wanakuwa njia panda hawawezi kujua mkweli nani? Mwisho wanaumme muoe usiutumie huu wimbo kuharalisha tabia chafu ya umalaya, pia dada zangu chonde chonde Mwana FA imewachongea ktk jamii inayotawaliwa na mfumo dume ambapo umalaya ni kwa mwanamke tu, wewe chunguza hata ktk ndoa nyingi wanaume wengi hata mabosi mpaka nyumba ndogo zao zinajulikana, kwani wewe unafikiri mwanamke yeye hana hisia au anamoyop wa chuma hapana lazima atarevenge tu, lakini nawasihi wanawake achana kushindana na wanaume kwani wao ndio wanapata support ya mfumo dume na kuamua nani na lini kuoa, hivyo badilisha tabia tulia,.

  22. Comment by karen on July 8th, 2008 2:06 am

    Thanks kaka Frateline
    yani wanaume wote wangekuwa waelewa kama ww basi kungekuwa hamna uhuni wala ukimwi usingeuwepo

  23. Comment by Belo on July 8th, 2008 6:50 am

    Binamu una AKILI baba
    Nafikiri ndio msanii wa TZ ambae unafanikiwa kila sekta
    Music
    Shule
    Maisha

  24. Comment by linda on July 8th, 2008 9:12 am

    KAZI KWELIKWELI
    Usioe ila unakoelekea ni kufa na ngoma, maana utakuwa unaoa usiku asubuhi uko single!
    hahahahaha ama kweli heri mjinga kuliko mpumbavu.

  25. Comment by bona mushi,cosfecaso on July 9th, 2008 2:43 am

    aissseeeeh!!! we AF ni NOMAA,yani ni bonge la dude la ukweliiiii!!.ila ukweli unabaki palepale mwanaume aogopi njaa jitose tuu mzeiiya.

  26. Comment by alpha on July 9th, 2008 3:44 am

    linda…hayo aliyoyaimba FA ni kweli kabisa!wat’ss yo problem ma’am??maana kwa jinsi anavyosema,hata ukioa aina ya mabo wanayofanya hao wadada lazima ufe kwa ngoma tu!ona haya kushabikia ukicheche…and stop hating!!

  27. Comment by Angel_Eyez on July 9th, 2008 7:42 am

    Wimbo umetulia ila tusisahau kwamba mwisho wa siku unavuna ulichopanda… hakuna mwanadamu anayetaka kuzeeka peke yake lazima upate mwenza wa kukuvua kivuvu (kukutoa upweke).
    Wanaume nao ni waongo pia ktk penzi; tatizo hakuna kuaminiana hivyo inakuwa tabu tu. Unakuta kila mmoja ameshaumizwa zamani na wa ubani wake basi hata akiwa ktk penzi jipya bado anajihami sana hata matokeo yake kupoteza penzi kwa kutokujiamini.

  28. Comment by Matty on July 10th, 2008 4:28 am

    Khaaaa!!!!! jamani sikupanga kusema lolote hapa lakini uvumilivu umenishinda hebu kwanza someni Mathayo 7:7 halafu nakuja.

  29. Comment by linda on July 14th, 2008 7:33 am

    hahaha matty umenichekesha
    usikimbie we wapige injili hao, vijana wanapaswa kubadilika
    sio sbb mwenzenu kaimba hivyo basi tena mnaiga si kila kitu cha kuiga jamani.
    Mathayo 7:7
    ”Ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtaona, bisheni hodi nanyi mtafunguliwa”
    Sasa watu hawataki kuomba wanataka tambarare tu haya, mtaishia ukicheche tu.

  30. Comment by linda on July 14th, 2008 7:40 am

    Alpha
    Endeleeeeeeeeeeaaaaaaaaaaaa

  31. Comment by hombiz on July 14th, 2008 6:12 pm

    Binti-mzuri, najua kuwa wanaume wazinzi nao wapo. Lakini kiwango chao sio kama cha vicheche!. Vicheche wengi saaana siku hizi!. Hata mimi yalinikuta na nimeshuhudia mengi toka kwa watu ninaowafahamu. I`m talking about super vicheche!
    Kaaaaaaaaaaaaaazi kweli kweli!

  32. Comment by Matty on July 15th, 2008 4:55 am

    Linda karibu tusomee uchungaji teh teh tetetetetetetett!

  33. Comment by linda on July 19th, 2008 3:45 am

    Asante Matty,
    Kila mtu anapaswa kujua why yuko duniani,
    hahahahaha,
    Umechagua fungu jema.

  34. Comment by angel on July 31st, 2008 9:04 am

    it has a good massege.congrats man.it take me more than 4hours simply listen to this true song.angel from IFM.TAKECARE GUYS BOTH GIRS AND BOYS ,MEN AND WOMEN.

  35. Comment by peter sigy on September 9th, 2008 2:52 am

    thats good F.A,kupata tunzo hile ilikua haki bro!

  36. Comment by FRED MUNGURE a.k.a OG on September 11th, 2008 7:41 am

    {PAMOJA NA KUZALIWA TANGA MAPENZI YALIKO ANZIA BADO NIPO NIPO MAMA} Mwana FA me nakukubali kinoma kwa mashairi,kwani hata mimi bado NIPO NIPO SANA………
    take 5 man

  37. Comment by halima on October 8th, 2008 8:39 am

    waswahili tunasema nyani haoni kundule, hata na sisi wanawake bado tupo tupo sana na fikiri tutafika.

  38. Comment by Mama wa Kichagga on October 31st, 2008 10:05 pm

    Nyimbo ya mfumo dume hii!

    Ungejiimba na wewe kuwa kicheche basi ungevuna sana ila kwa kuwa ktk mrengo wa kushoto na kutuhukumu sisi peke yetu ulikosea sana!

    Hivi huyo demu anajichechea mwenyewe? si kuna ki-mwana FA pembeni?

    NB: Hivi unajua wanawake ni asilimia ngapi TZ au duniani? Kwa kukisia ni sawa na 50%. Huoni hapo kwa kuimba huu wimbo wa kuipotosha jamii unaathiri 50% ya soko la bidhaa zako?

    Think twice & use common sense next time kabla ya kufyatua wimbo na epuka lugha zinazokandamiza jamii fulani. Jua wewe ni kioo hivyo jamii inategemea uimulike kwa haki na sio namna hii hapa! Please bring your school forward au unadesa?

  39. Comment by nunku on November 5th, 2008 1:15 pm

    FA najua umekomaa kimashairi na haiwezekani kuandika nyimbo yenye ujumbe na hisia nzito kama hii bila kuguswa na kitu au kufikwa na jambo[mfano Jnature ilimuuma sana alipotendwa na cnta] sasa wewe nani kakufilimba mtima wako mpaka ukaamua kutuburudisha namna hiyo mwana? FA kwenye kideo yule binti ananichanganya ni mama yako au ni mama yako mdogo?

  40. Comment by Elibahati on December 11th, 2008 4:28 am

    Ebwaba Fa we Noma japo watu wana jib ila waache hawana mistari!

  41. Comment by Fifi on January 6th, 2009 9:53 am

    sina la zaidi kwa hayo ndugu yangu Frateline amesema apo ju kidogo ni ukweli kabisa. ungera sana Frateline.

  42. Comment by monrasi on February 1st, 2009 9:35 am

    mimi nilihonga simu nikajikuta nimeoa. Lakini sasa nasumbuka kinoma. MAMA HASHIKIKI TENA.

Leave a Reply