

Kitimtim kinaendelea kutimka huko mjini Dodoma.Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini wa sasa,Nazir Karamagi(pichani kushoto) na Waziri wa zamani wa wizara hiyo hiyo ambaye hivi sasa ni Waziri wa Afrika Mashariki,Dr.Ibrahim Msabaha(pichani kulia) nao wametangaza azma yao ya kujiuzulu.Wameshamwandikia Rais Jakaya Kikwete nia yao.Kazi kweli kweli.
Picha kwa hisani ya Bernard at Bongo Pixs
Feedback / Comments
17 Responses to “KARAMAGI NA MSABAHA NAO WATANGAZA KUJIUZULU”
Leave a Reply


Duuhh hi kali, mimi naamini kuwa hakuna atayekubali kuhusika moja kwa moja na Richmonduli, ila Tanzania tumefika mahali tuseme baasiii inatosha kwa hawa viongozi wanafki. by the way luku ya elfu 15 ilinitosha kwa mwezi, sasa inabidi ninunue wa elfu 30, wakati sijaongeza hata pasi ya umeme.
Mfano mzuri, pamoja na kujiuzuru kwao bado sheria ichukue mkondo wake.
Mi nashauri tu baraza la mawaziri liwe restuctured, wabadhilifu bado ni wengi tu. Utashangaa waziri akijidai mwaminifu na mzalendo mchapa kazi, anapuuzwa au kuondolewa, kuna watu safi na wachapa kazi kabisa kama alivyokuwa mrema wa enzi hizo, lakini utashangaa majambazi ndo yanapewa office. Sasa hawa watu wameshachafua CV ya JK kabisa hata ccm pia. wafanyabiashara wakubwa ndo wamezishika hatamu za chama. kodi ya umeme juu, maisha ya mtanzania ICU, pamoja na migodi ya dhahabu na almas, na gemstones. Inabidi sheria iundwe wafirisiwe hawa maana wamejirimbikizia.
Ama kweli hiyo ni taarifa ya RICH-MONDULI! Karamagi umeingia mkataba wa madini kinyemela kumbe ulikuwa unajazia za RICH-MONDULI! Du! ulikuwa na mikakati mikali, na brother MSA-SHABAHA ulienga vibaya au ni shabaha imekwishwa? Aroo! hiro rijamaa riperekwe range rikajifunze tena kurenga shabaha, na kweli kaka, ukapelekwa EAST AFRICA kama waziri! Sasa sijui kama na huko ulilenga au ulikosea! Kujiuzulu haitoshi! Hakya mungu nawaambia nyie siku mtakufa huko motoni nyie mtageuzwa kuni za kuwachoma wadhambi wengine!
Wote majizi watupu na bado!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Sasa baada ya kujiuzulu nini kinafuata, isije ikawa kama Dalali, wachukuliwe sheria ala!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
hii RICHMINDS sory RICHARD MONDULI i mean Richmonds ni kitu kidogo sana kati ya mauozo yaliyoko uko tungeje tu tujionee
walisema wahenga
“U can fool all the peolpe some of the time, you can fool some of the people all the time but you cannot fool all the people all the time”
mafisadi wanaujua huu
“Bangusilo” mie chambilecho Msabaa
wawe Kilongola kweli.
Huyu NaE Na miwani yakeeeeeehadi nakosea spelling.mihela yote hiyo ya migodini ona walivyochoka mashavu!!!!!RUDISHENI MALI ZA UMMMAAAAAAAAAA WAFILISIWE!!!!!!!
Machoni kama watu…..
Hamna tofauti na wauaji..,mmepalilia umasikini Tanzania kwa uroho na ubinafsi wenu. Hospitali hazina dawa, shule hazina vifaa vya kutosha, maisha yanazidi kuwa magumu n.k. Kila kukicha inakuwa afadhali ya jana..!
Tanzania iliyopata uhuru miaka karibia 50 iliyopita bado inapigana na adui ujinga, maradhi na umasikini…!
Milikuwa watu wa kuhubiri msiyoyatenda na kuliigizia taifa hasara isiyoelezeka wala kuingia akilini.
MAFISADI WAKUBWA.
Naomba kuuliza…,
Hivi hawa nao ni bongo celebrities au?
Jamani tunapoongea hapa tupige picha kule vijijini! Achilia mbali mijini ambako watu wanashindwa kumudu hata mlo mmoja! Hela waliyokuwa wanalipana kwa mwezi @ mtu mmoja ingetosha kabisa kuwalipa social benefit allowance WaTZ milioni 4 @ mtu sh. 30,000/mwezi sawa na sh. 120,000,000,000 kwa nchi nzima!
Hii changamoto [wind of change] lihamie ndani ya mawizara na idara zote za serikali na watu binafsi kama kweli tunamedhamiria kupambana na ufisadi kwani huko ndiko visima na chemichemi za ufisadi. JK yaani ni vijikundi vya mafisadi vimejitega kila mahali vikiamini bila mission town maisha hayaendi. Watu wanaishi kama mtoto wa mama na mototo wa kambo yaani ni unyama unyama tuu. Chunguza utapata majibu haya yote na kuzidi.
NB: Mh. JK Watu wanahasira si vijijini si mijini si maofisini maana mambo yanayotendeka na hali ya maisha ilivyo ni mabaya sana.
Wito: Chagua baraza la mawaziri ambalo linaweza kuueleza umma wa Watanzania wamewahi kuufanyia nini hadi waweze kupata hizo nafasi na pia WATAWAFANYIA NINI WATANZANIA TOFAUTI NA WENZAO WALIOWATANGULIA?. Ikiwezekana unapompendekeza mtu kabla hujampitisha awasilishe ripoti ya utendaji wake kwa maandishi na mkakati anaotarajia kuufanya.
KWANINI TUSIUTANGAZE MWAKA 2008 KAMA MAALUMU KWA KAMPENI YA KUPAMBANA NA UFISADI TZ? YAANI KAZI KUBWA IWE HIYO ILI MWAKANI TUFANYE KAZI KTK MAZINGIRA YA HAKI?
Mimi kutoka moyoni kwa moyo wangu huu wa kimasikini na jinsi riport ilivyoniumiza. NAWAHAKIKISHIA WANAINCHI WOTE LAZIMA NIWASHUGHULIKIE KIKAMILIFU KAMA HAWATA PELEKWA KWENYE VYOMBO VYA SHERIA ILI WAWEZE KUFUNGWA. ROHO INANIUMA SANA KUONA BADO WANAENDELEA NA UBUNGE WAKATI SIFA ZA KUWA WABUNGE HAWANA. LOWASSA *** SANA WEWE, SIO MZALENDO KABISA. SASA HAMNA WALINZI WA HALI YA JUU, NITAJITOA MUHANGA KWA AJILI YENU
[...] and Minerals Nazir Karamagi and the Minister for East African Cooperation Dr. Ibrahim Msabaha by Bongo Celebrity and Charahani [...]
Lione hilo li haya HALINA HAYA >>>>>>>>>
LINAKULA MALI YA UMMA
na bado yai kweli mwizi siku zake 40 lili anzia wazo Cement company likaingia Bandari TITCS sasa likae3nda hukoooo….
Afilisiwe na Majangili wenzake
bado wengine akina Diallo ,Mramba,YONA, ROSTAM nawengine yapo majizi mengi
HUyu Lowasa nilijua hata fikka mbali maana amezidi na Ule ubalozi wa south africa ni jengo lake afilisiwe haraka ili kodi iingie serikalini na si kwenye acc. yake
MWIZI mkubwa
namshukuru saaana mama malecela maana nikiwa bongo nilisikiliza kikao cha bunge kujadili Ripoti ya DR MWakembe yani mama alikuwa mkali sana na ameapa kutokomeza ufisada
Hongereni wananchi wa jimbo la same mashariki kwa kuwa na MBUNGe dawa
kwekli tukipata wanawake 10 kama hao tutafika mbali
Ila kikwete bado anazuga
hakumteua mama huyu wala mwakyembe kwenye baraza lake
we mwache tu aendelee kucheza na watanzania
Yaani hawa mafisadi waliokubuhu wafanywe kitu mbaya sio wanaachwa hivi kiulaini sheria ichukue mkondo wake.
hivi ni kwa nini serekali yetu inapenda kulindana nadhani wanashiriki nao kufanya maovu, ila naamini mkono wa mungu utawaumbua hakuna chenye mwanzo kisichokuwa na mwisho.
mimi hata kama wakifia jela naona sawa tu.mmekula vya kutosha hukumu yenu imeandaliwa kama si na binadamu basi na mungu
majizi wakubwa nyie hizi ni nyakati za mwisho mtatajana tu bila kulazimishwa na mtu na naomba kwa ajili yenu,hivi ww huoni hata aibu unakula jasho la mwenzako nakufananisha na mwanaume anayelishwa na mwanamke
haoooooo!!!!!! wanaume wazima na elimu yenu mnaiba aibu
mnaaibisha familia zenu wanashindwa pa kuweka nyuso zao.