Kama yupo msanii ambaye kwa sasa,kwa maoni yangu,ndiye balozi mzuri wa Afrika nchini Marekani,basi mwanamuziki huyo ni Akon.Huyu jamaa ni mwafrika kwanza kabla ya mambo mengine.Anaupenda uafrika na hafichi.Kila analolifanya anataka ijulikane wazi kwamba kwao ni Afrika.Mtizame katika wimbo huu wa hivi karibuni unaoitwa Oh Afrika.

Miezi saba baadaye,aliyekuwa daktari wa Mfalme wa Muziki wa Pop ulimwenguni,Michael Jackson, Dr.Conrad Murray ameshtakiwa rasmi kwa kifo cha mwanamuziki huyo maarufu ambaye katika maisha yake,aligusa wengi.Michael Jackson alifariki dunia tarehe 25 June mwaka jana akiwa na umri wa miaka 50.
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari, Dr.Murray ambaye alifikishwa mahakamani mchana huu huko Los Angeles,amekana shtaka lake na ameachiwa kwa dhamana ya dola 75,000. Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa tena tarehe 5 April.
Ndugu wa Michael Jackson,kaka zake Jermaine,Tito,Jackie na Randy ,dada yake LaToya na wazazi wake Joe na Katherine walikuwepo mahakamani kusikiliza kesi hiyo.
Hapo kabla Dr.Conrad Murray ambaye ni mzaliwa wa nchini Grenada,alikiri kwa polisi kwamba alimchoma Michael Jackson sindano ya dawa aina ya Anaesthetic Propofol kwa dhumuni la kumsaidia bingwa huyo wa Pop kulala.Alisema aliporudi tena chumbani alimkuta Michael akiwa hapumui.
Mchunguzi wa vifo wa Los Angeles alithibitisha baadaye kwamba dawa hizo ndizo zilizosababisha kifo cha Michael Jackson. Dr.Murray alikuwa ameajiriwa maalum kwa ajili ya kumuandaa Michael Jackson katika tour iliyokuwa ijulikane kama This Is It ambayo ilikuwa ianzie nchini Uingereza.

Hamis Ramadhan,maarufu kama H-Baba(pichani) yawezekana sio jina geni kwako.Huyu ni miongoni mwa wanamuzuki waliojikita katika mtindo ujulikanao kama TAKEU(Mr.Nice ndiye anasemekana kuwa mwanzilishi wake).
Ambacho unaweza kuwa hukijui ni kuhusu “imani” aliyonayo. Hivi karibuni H-Baba alinukuliwa na chombo kimoja cha habari akisema kwamba amelogwa na mmoja wa wasanii wenzake kitu ambacho anadai ndicho kilichosababisha mambo yake kwenda ‘kombo” katika siku za karibuni.
Kwa masikitiko na upole,H-Baba amenukuliwa akisema “Unajuwa mtu ataniona mimi kama naongopa lakini ukweli ni kuwa nilichezewa ila nilikuwa sijui nimekuja kugundua baada ya kupita pita kwenye tiba.Nilianza kujihisi hivyo mara baada ya kugombana na watu wengi sana nikiwa sijielewi”
H Baba anakiri kwamba hivi sasa ameshapona kutoka katika matatizo yaliyokuwa yakimsumbua baada ya kupata tiba toka kwa wataalamu wa miti shamba.
Bila kumtaja wazi huyo ‘mchawi” wake H-Baba alizidi kusema ” Unajuwa ni ukweli kabisa waswahili hawakukosea walivyosema kikulacho kinguoni mwako, kwani yote hayo yalikuwa yakifanywa na mtu wa karibu kabisa tena rafiki yangu mkubwa”.
Mfano mmojawapo wa matatizo yake,anasema “Matatizo mengi yalitokana na Irene(Uwoya), unajua watu wengi hawakupenda niwe na Irene, kwahiyo ili kunikomoa ikabidi waniroge, mimi na Irene tukawa hatuelewani, tunagombana mpaka tukaachana,”
Je,unaamini kwamba ni kweli yawezekana H-Baba amefanyiwa anachodai kufanyiwa au hii ni “publicity stunt”?
Ujasiriamali ndio neno jipya. Kila mtu anaongelea habari za ujasiriamali. Pengine hii inatokana na wengi wetu kutambua kwamba nyakati zimebadilika na ujasiriamali ndio njia iliyo sahihi zaidi kama mtu anatamani mafanikio ya kweli maishani.Vijana ndio chachu zaidi ya ujasiriamali au naweza kusema ndio wanategemewa zaidi kuendeleza ujasiriamali hususani katika ulimwengu wa leo wa sayansi na tekinolojia.
Pamoja na nia nzuri walizonazo vijana, pengine ukiwemo wewe unayesoma makala hii, kipo kizingiti ambacho ni lazima watu wajifunze mbinu mpya za kukivuka. Kizingiti hicho ni aina ya elimu itolewayo mashuleni. Kwa bahati mbaya elimu zitolewazo mashuleni bado hazijawekwa katika msingi unaomuwezesha kijana kujiajiri au kwa maneno mengine kuwa mjasiriamali pindi amalizapo masomo yake.
Bado tupo katika ule mfumo wa kikoloni. Ukimaliza shule unachotakiwa ni kuanza kutafuta kazi. Zunguka jijini Dar-es-salaam kwa mfano, utakutana na vijana wengi wasomi waliohitimu katika vyuo vikuu mbalimbali nchini wakiwa wamebeba vyeti vyao kwenye vijifuko vya plastiki wakizurura kusaka ajira. Hakuna anayefiria kujiajiri kwa kutumia elimu aliyoipata chuoni. Kwanini? Ndivyo ilivyo. Elimu aliyopewa haikumuandaa.Utakutana na engineer wa umeme ambaye hajawahi kubadilisha hata balbu!(nimeongeza chumvi kidogo hapa lakini kuna ukweli ndani yake!) Amesomea nadharia zaidi ya vitendo. Utakutana na mwanafunzi mhitimu wa masomo ya kilimo na mazingira ambaye hajui shamba ni nini.Hilo ni kosa katika mfumo wetu wa elimu. Ni lazima serikali ichukue jukumu la makusudi kubadili mfumo huo.
Lakini wapo wengine wengi ambao wana nia ya kweli ya kuwa wajasiriamali. Wana nia ya kujiajiri. Leo tutaangalia jinsi gani mjasiriamali chipukizi aanzishe kampeni yake. Si ushasikia kwamba biashara siku hizi ni kujuana? Ujasiriamali pia. Ni muhimu sana kujua ni nani au ni wapi uende endapo mambo yatakwama. Siongelei wapi uende kutoa au kupokea rushwa.La. Nataka kuongelea kitu kinachoitwa na wenzetu wa magharibi “networking”.Kwetu sisi hiki ndicho tunachoita “mtandao”.Mitandao ya kijamii kama vile facebook,twitter,myspace nk ni sehemu nzuri ya kutengeneza network.Itumie vizuri.
Ni muhimu kutengeneza mtandao mzuri kama unataka kuwa mjasiriamali makini na hususani kama unataka kufanikiwa. Kumbuka kwamba hapa hatuongelei kubadilishana business cards peke yake bali kumjua mtu kwa nia njema ya kusaidiana.Kumbuka neno ni “kusaidiana” na sio wewe pekee kupokea msaada.Lazima pawe na nia njema ya kusaidiana.
Kabla sijaanza kuorodhesha mbinu mbalimbali za kutengeneza ‘mtandao’ wako, naomba nikwambie kwamba siri ya kwanza ya kuanza kuwa mjasiriamali ni maandalizi.Jiandae kwa mtaji,elimu(ya darasani na mtaani),mbinu za kibiashara nk. Pili hakikisha kwamba una mapenzi ya dhati na hicho unachotaka kufanya.Usiingie kwenye biashara au ujasiriamali kwa sababu tu umemuona fulani amefanya hivyo.Kuna umuhimu mkubwa wa kujitambua katika suala zima la ujasiriamali. Baada ya kusema hivyo,sasa tuingie kwenye maeneo ya kutengeneza mtandao wako kama mjasiriamali;
- Washindani wako: Biashara ni ushindani lakini sio uadui.Kama unataka kuwa mjasiriamali mwenye mafanikio ni vizuri sana ukawajua washindani wako wa kibiashara.Pata vipeperushi vyao,tembelea tovuti zao,wajue wateja wao na kwanini hao watu ni wateja wao.Kisha jitambulishe kwao.Najua hapa unasema;nijitambulishe?!! Ndio,jitambulishe.Kama nilivyosema ni washindani lakini sio maadui zako. Mshindani wako anaweza kukufaa pia.Anaweza kuzidiwa na kazi akakusukumia zingine.Jitambulishe,jenga uhusiano mzuri wa kibiashara.Isitoshe nyote mpo kwenye biashara moja,sekta moja.Ya kesho hamyajui.Kama kuna chama au ushirika wa watu waliomo kwenye eneo lako la ujasiriamali,jiunge. (more…)

Mara ya kwanza tuliwasiliana mwaka jana.Akanieleza mipango yake,ndoto zake na mikakati aliyonayo katika kutimiza ndoto zake.Kama ilivyokuwa kwa mamilioni ya watu ulimwenguni, Babu Sinare ambaye kisanii anajulikana kwa jina la Albino Fulani, alikerwa na kuhuzunishwa na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi(albino) kwa imani za kishirikina. Kwake yeye,ilikuwa ni kama vile wametonesha kidonda ambacho alidhani kilishapona kwani Babu Sikare ni albino pia.
Miongoni mwa mipango yake ilikuwa ni pamoja na kuanzisha NGO yake ambayo italenga kusaidia albino wengine.Kupitia muziki wake,aliahidi kwamba atazidi kukemea mauaji ya albino.Hakuwa anatania.Alianzisha shirika lisilo la kiserikali na kuliita Afro-Bino. Matunda ya shirika hilo yameanza kuonekana.
Pichani juu ni Babu Sikare(kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi wa Huduma za Hospitali kutoka Wizara ya Afya, Dr. Magreth Mhando (kulia) karatasi yenye maelekezo ya msaada wa mafuta ya kuzuia ngozi isiharibike na jua kwa ajili ya watoto wenye ulemavu wa ngozi Tanzania (Albino) yenye thamani ya dolla 1,500. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ustawi wa Jamii Bi. Magreth Njimba.
Kutoka moyoni,naomba kumpongeza Babu Sinare na shirika zima la Afro-Bino.We salute you and we support you.
Albino Fulani anatamba pia na wimbo wake Barua Kwa Mama.Bonyeza hapa kuusikia.
Kama wewe ni mtizamaji au mpenzi wa sinema za kutoka nchini Nigeria,bila shaka umewahi kuwaona wachekeshaji wawili wajulikanao kama Aki na Ukwa.Wanasemekana ndio waigizaji wafupi kuliko wote nchini humo.Habari nzuri,kama wewe unapendezwa na vichekesho vya Aki na Ukwa ni kwamba wapo njiani kuja jijini Dar-es-salaam.
Kwa mujibu wa Gazeti la Mwanaspoti,wachekeshaji hao wanatarajiwa kufanya vitu vyao katika tamasha la watoto yatima, na wale wanaoishi katika mazingira magumu Februari 14 mwaka huu. Tamasha hilo linatarajiwa kufanyika siku ya wapendanao(Valentine’s Day) katika viwanja vya TTCL, Kijitonyama jijini Dar es salaam.
Aki na Ukwa watakuwa nchini kwa lengo wa kucheza na kufurahi na watoto mbalimbali wahishio kwenye mazingira magumu.
Watasindikizwa na wasanii wengine wa ndani wanaotarajiwa kutumbuiza katika tamasha hilo ni pamoja na Ze Comedy, Q-Chief, Mr.Nice, Rose Mhando na Mrisho Mpoto. Kwa habari zaidi bonyeza hapa.

Miongoni mwa matukio ya ki-muziki ambayo yataendelea kukumbukwa kwa muda mrefu ni pamoja na tukio la jumla ya wanamuziki 45 kukusanyika katika studio za Jim Henson za jijini Los Angeles mwaka 1985 na kutengeneza wimbo ulioitwa We Are The World ambao ulikuwa mahsusi kwa kuchangia fedha kwa ajili ya Afrika na hususani nchi ya Ethiopia ambayo ilikuwa imekumbwa na ukame wa kutisha kuanzia mwaka 1984-1985.Ulikuwa ni umoja na upendo wa aina yake waliouonyesha wanamuziki wale sio tu kwa bara la Afrika bali kwa taasisi nzima ya ubinadamu. Wanamuziki Lionel Richie na Michael Jackson(RIP) ndio walioandika wimbo ule ambao ulifanikiwa kuchangisha jumla ya dola milioni 30 zilizokwenda kusaidia waathirika wa ukame ule.
Katika kujaribu kurudia kile walichofanya superstars wa ulimwengu wa muziki takribani miaka 25 iliyopita, hapo juzi jumla ya wasanii 100 (wengi wao kutoka Marekani) ambao wanatamba hivi sasa katika muziki ulimwenguni,walikusanyika katika studio moja chini ya Producer yule yule aliyefyatua We Are The World ya mwaka 1985,Quincy Jones ili kuutengeneza upya wimbo wa We Are The World(remake of We Are The World). Lakini safari hii sio kwa ajili ya kuchangia Afrika bali ndugu zetu wa Haiti ambao kama unavyojua wiki chache zilizopita nchi yao ilipata tetemeko la ardhi ambalo linahofiwa kwamba lilichukua maisha ya jumla ya watu 200,000.
Original We Are The World.
Baadhi ya wanamuziki wenye majina makubwa ambao wamo katika We Are The World mpya ni pamoja na Wyclef Jean, Kanye West,Celine Dion,Jennifer Hudson,Miley Cyrus,Barbra Streisand,Tony Bennett,Jamie Foxx,Natalie Cole, Akon, Carlos Santana,Josh Groban,Justin Bieber(kijana wa miaka 15 raia wa Canada,alikuwa hajazaliwa huyu mwaka 1985), Snoop Dogg,Drake,LL Cool J na hata Rapper Lil Wayne ambaye anasema alidhani wanamtania alipoambiwa kwamba anahitajika “kuimba”.
Wengine ni kama vile Usher,Jonas Brothers,Pink, Gladys Knight,Wil.i.am,Brandy,Keri Hilson,Busta Rhymes,T-Pain,Robin Thicke,Trey Songz,Adam Levine,Tyrese na wengine kibao.Nitaendelea kuongeza majina ya washiriki wengine katika orodha hii kwa kumbukumbu ya vizazi vijavyo.
Janet Jackson(dada wa Michael Jackson) ambaye hakuwepo studio anatarajiwa kuimba sehemu ya marehemu kaka yake kabla ya kutolewa rasmi kwa video ya remake hii ya We Are The World ambayo inatarajiwa kuonyeshwa rasmi tarehe 12 mwezi huu katika kituo cha televisheni cha NBC cha nchini Marekani kwenda sambamba na ufunguzi wa michezo ya Olympics ya majira ya baridi(Winter Olympics) inayofanyikia huko Vancouver nchini Canada kwa mwaka huu. Video ya wimbo huu mpya imeongozwa na Director wa movie ya Crash(kama hujaiona fanya bidii uione),Paul Haggis.
Je unadhani kuna uwezekano wa wimbo huu uliotengenezwa upya,kuushinda ule wa zamani au kupata mafanikio zaidi ya original? Kuna watu wanasema ni vyema kwamba Lionel Richie na Quincy Jones wapo kusimamia na kuhakikisha kwamba the “1985 spirit ” inabakia pale pale lakini bila kuwepo kwa Michael Jackson ni pengo kubwa sana.Wewe unasemaje?
Photo/Kevin Mazur/wireimage.com. Kwa picha zaidi bonyeza hapa.
Unapoongelea sinema,hakuna ubishi kwamba majadiliano yako inabidi yaanzie Hollywood.Na unapokuwa Hollywood na kuamua kuanzisha mjadala wa Tuzo(awards) basi yakupasa uanzie kwenye tuzo maarufu za Academy au Oscars.
Muda mchache uliopita majina ya sinema,waigizaji,waongoza sinema na vipengele vingine walioteuliwa kuwania tuzo hizo kwa mwaka huu yametangazwa. Kama ambavyo ilitarajiwa, sinema ya Avatar iliyoongozwa na James Cameron pamoja na sinema ya The Hurt Locker ambayo imeongozwa na Kathryn Bigelow(mke wa zamani wa James Cameron) ndio zimepata teuzi nyingi zaidi katika kuwania tuzo hizo maarufu ambazo zinafanyika kwa mara ya 82 (miaka 82). Movie hizo zimeteuliwa mara 9 au katika vipengele 9.
Shughuli za mwaka huu za tuzo hizo zinatarajiwa kufanyika tarehe 7 Mwezi Machi(takribani siku 33 zijazo).Zitaonyeshwa moja kwa moja(live) kupitia kituo cha televisheni cha ABC cha nchini Marekani.
Kwa orodha kamili ya Oscar Nominations kwa mwaka huu,bonyeza hapa. Je kuna movie,actor au actress ambaye ulitarajia angeteuliwa kuwania tuzo za mwaka huu ambaye hajatokea katika orodha?

Yapo majina ya wasanii wa kizazi kipya ambao ukisikia wameshirikiana(collaborate)kutengeneza kazi fulani, basi unakuwa na imani kubwa kwamba kazi hiyo ina nafasi kubwa ya kuwa nzuri. Hiyo inatokana na uzoefu na pia zingatio za kazi zao zilizopita,nafasi waliyonayo katika uwanja mpana wa sanaa ya muziki na mambo kama hayo.
Hivi karibuni nilipoletewa kazi mpya na kuambiwa kwamba wasanii waliomo katika kazi hiyo ni TID(Top in Dar) na Chid Benz, nilikuwa na uhakika kwamba kazi hiyo itakuwa imesimama.TID na Chid ni miongoni mwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao binafsi nawaheshimu na sioni noma kusema kwamba nazipenda nyingi kati ya kazi zao.Habari nzuri ni kwamba hawakuniangusha katika kazi hii ya hivi karibuni inayokwenda kwa jina Huyu.
Kama zilivyo kazi nyingi za wasanii wetu siku hizi,hii pia ni hadithi ya mapenzi (bado natamani wigo wa yaliyomo(content) za kazi za wasanii upanuke zaidi na kugusa maeneo mengine yanayoizunguka jamii).Kinachoufanya wimbo huu uwe tofauti ni uwezo binafsi wa wasanii husika na hadithi yenyewe.
Kazi hii imepikwa pale Tetemesha Records(kule kule alikoibukia Hussein Machozi) chini ya George Mpanda au maarufu kama Kid Bwoy. Bonyeza player hapo chini usikilize wimbo Huyu.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Tuzo maarufu za muziki za Grammy zimemalizika muda mfupi uliopita jijini Los Angeles.Kama kawaida ya tuzo maarufu kama hizo,huwa kuna kuvunjwa kwa rekodi au kuwekwa rekodi mpya,vituko mbalimbali, mavazi ya kukumbukwa na pia performances za kukumbukwa.
Kwa mwaka huu,rekodi mpya imewekwa na Beyonce Knowles.Binti huyo ambaye ni mke wa rapper maarufu ulimwenguni,Jay-Z ameibuka na jumla ya tuzo sita na hivyo kuweka rekodi ya kuwa mwanamuziki wa kike wa kwanza kushinda idadi hiyo ya tuzo katika usiku mmoja wa tuzo za Grammy!
Kwa upande wa performances ambazo nitazikumbuka kwa muda ni pamoja na performance aliyofanya Pink huku akijibinubinua hewani kwa kutumia kipande cha nguo! Kuna haja ya kuchunguza zaidi ili kujua kiasi gani cha ile performance ni kweli na kiasi gani ni uzushi.It was hot though.
Nyingine niliyoipenda ni performance ya Lil Wayne(yuko mbioni kwenda jela kwa miezi nane na huenda hii ilikuwa ni performance yake ya mwisho), Drake na Eminem. Nilifurahi kumuona Eminem akiwa bado yupo fit na huku uwezo wake wa kumiliki jukwaa ukiwa pale pale.Hapo katikati alipotea kutokana na matumizi ya kutisha ya madawa ya kulevya.
Mavazi: Mimi sio mtaalam sana wa mambo ya mavazi.Lakini hata hivyo hiyo haikunizuia kuona kwamba Lady Gaga alitia fora kwa kivazi alichovaa baada ya ku-perform na kuungana na wenzake katika audience.Sijui bado jina la kitu alichovaa;ni gauni au?
Kwa ujumla tuzo kubwa kubwa zilienda kama ifuatavyo;
- Record of the Year – Kings of Leon – “Use Somebody”
- Album of the Year – Taylor Swift – ‘Fearless’
- Song of the Year – Beyonce – “Single Ladies (Put a Ring On It)”
- Best New Artist – Zac Brown Band
- Best Female Pop Vocal – Beyonce – “Halo”
- Best Male Pop Vocal – Jason Mraz – “Make It Mine”
- Best Duo or Group With Vocals – Black Eyed Peas – “I Gotta Feeling”
- Best Pop Vocal Album – Black Eyed Peas – ‘The E.N.D
Kwa orodha kamili ya washindi,bonyeza hapa.

