Baada ya kuukosa Ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa miaka kadhaa kwa kupoteza katika fainali mbili kati ya tatu zilizopita, hatimaye timu ya Bayern Munich imefanikiwa kuutwaa ubingwa huo baada ya kuishinda timu ya Borussia Dortmund kwa jumla ya magoli 2-1 katika mchezo wa fainali uliopigwa katika Uwanja wa Wembley jijini London nchini Uingereza.
Magoli kutoka kwa Mario Mandzukic katika dakika ya 60 na la pili kutoka kwa Mholanzi Arjen Robben kunako dakika ya 89 ndio yaliyopeleka shangwe na vifijo kwa mashabiki wa Munich. Kabla ya hapo kunako dakika ya 68 Dortmund walikuwa wamesawazisha kwa goli ya penati liliwekwa wavuni na Ilkay Guendogan.
Ushindi huo wa Bayern unayaweka wazi matumaini yao ya kuwa na mwaka wa aina yake katika mafanikio kwani timu hiyo imeshatwaa Ubingwa wa Ligi ya Ujerumani (Bundesliga) na Jumamosi ijayo watavaana na VfB Stuttgart katika fainali ya Kombe huko mjini Berlin.
Umesikia fununu na hisia.Nani ataiwakilisha Tanzania? Nakuhakikishia ni fununu na hisia tu. Jiandae Kushangaa!!
Ujumbe uliowekwa kwenye e-mail iliyoniletea wimbo huu imenisihi kwamba nitoe support kwa wimbo bora wa mwaka. Ukweli ni kwamba unapopokea ujumbe kama huo, unajiuliza maswali kadhaa.Eeenh! Kwanini? Nani kaimba nk. Nilipousikiliza (mara mbili) nimeona kweli kuna kitu ambacho kinaubeba. Lakini mimi ni mdau mmoja. Kuna wewe msomaji na mpenzi wa muziki. Usikilize hapo chini na bila shaka nawe utakuwa “Judge”
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
*DETAILS*
*TRACK NAME: UMENIPOTEZA
ARTIST NAME: INNOCENT MKUMBA
COMPOSED BY INNOCENT
PRODUCER: TIDDY HOTTER
STUDIO: ONE LOVE FX

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Song;Bye Bye
Download Link; http://www.hulkshare.
Je, unajiamini kuwa na kitu kinachokufanya uwe mkali mtarajiwa? Vodacom inatafuta mtangazaji mpya wa kipindi cha TV kitakachoanza hivi karibuni. Soma namna ya kushiriki na unaweza kuwa mmoja ya watangazaji wa kipindi hiki.
Kazi ni kwako.
Jumamosi imekaribia. Mashabiki wa soka duniani wanalo la kuzungumzia, kujadili na kisha siku ya siku kujumuika kwa pamoja kushuhudia mechi kali na ya aina yake. Ni fainali ya Kombe la UEFA baina ya timu mbili kutoka Ujerumani Bayern Munich wakipambana na Borussia Dortmund.
Fainali hii ambayo itafanyikia jijini London nchini Uingereza katika uwanja maarufu wa Wembley, inazikutanisha timu mbili kutoka Ujerumani ambazo zilitinga fainali hiyo baada ya kuiangusha miamba ya soka toka Hispania, Real Madrid na Barcelona. Real Madrid walipokea kipigo cha 3-1 nchini Ujerumani na ingawa katika mechi ya marudiano Real Madrid walishinda bao 2-0, Borrusia Dortmund wakasonga mbele.
Kwa upande wa Bayern Munich wao waliingia kwa kishindo zaidi baada ya kuwachapa Barcelona jumla ya bao 4-0 katika mechi ya kwanza na 3-0 katika marudiano pale Nou Camp.
Je,ni nani ataibuka mshindi katika fainali hii? Ni Bayern Munich au Borussia Dortmund? Usikose kutizama kipute hiki kupitia DStv pekee!
Huu wimbo ulitoka rasmi wiki iliyopita. Kwa makusudi sikuuweka hewani. Nilikuwa na bado nina maana yangu. Ukiendelea kusoma bila shaka utanielewa.
Kila kizazi kina tabia au haki ya kudai kwamba muziki wao, wa enzi zao, ni bora kuliko wa kizazi kingine. Bila shaka hilo halikushangazi. Ulitegemea kizazi fulani kiseme kwamba chao kilikuwa au ni cha mbumbumbu wasio wabunifu wala wenye kuchangamsha akili zao na kutengeneza vitu vya nadra?! Sidhani….mwamba ngoma huvutia upande wake. Ni hulka ya binadamu.
Lakini historia ya binadamu inaonyesha kwamba mahali ambapo binadamu alifanya vyema zaidi ni pale aliposhirikiana na wenzake.Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Bila shaka kuna kila aina ya ukweli katika hili.
Kwenye sanaa ya muziki nchini Tanzania, miongoni mwa wasanii ambao wameamua kwa makusudi kuileta dhana hiyo kwa vitendo ni MwanaFA. Yeye(na nakubaliana naye kabisa) anaamini kwamba kila kizazi kina yake mazuri. Cha msingi ni kuendeleza yale mazuri na kuachana na yale ambayo hayana maana. Kuna muziki mzuri kutoka kizazi kile. Kuna muziki mzuri kutoka kizazi hiki.Kwanini tusichanganye tukapata kizuri zaidi? Ameeita kampeni yake Keeping The Good Music Alive.
Hicho ndicho alichokizangatia alipotoka na Yalaiti ikiwa ni maingiliano ya enzi zile za Sitti Binti Saad na sasa. Linah akaingia na kukoleza ya kale na mapya. Huu hapa sasa ni ujio wake katika wimbo Kama Zamani akiwa amewashirikisha The Kilimanjaro Band (Njenje) na Mandojo & Domokaya.
Sasa kwanini nimesubiri mpaka leo kuweka post hii? Ni hivi; naunga mkono harakati hizi za MwanaFa za Keeping The Good Music Alive. Niliona kwa sababu naunga mkono juhudi hizi, basi nisubiri kwanza kibao hicho kipatikane kwenye platforms mbalimbali za mtandaoni ambapo na wewe unaweza kuunga mkono jitihada zake kwa kuununua copy yako.Usikilize hapa chini…lakini kama unaamini kwamba muziki mzuri unahitaji maandalizi mengi na yenye kugharimu, basi tafadhali ungana nami katika juhudi za kuwasaidia wasanii wetu(akiwemo MwanaFA) kwa kununua kazi yake.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Naam unaweza kununua wimbo huu kwa kufuata Links hizi.Kumbuka ORIGINALS ARE MASTERPIECES.Let’s support our artists(especially those who makes good music). Nunua kupitia Links Zifuatazo;
KUNUNUA KUPITIA AMAZON BONYEZA HAPA
Wasanii mbalimbali kutoka Nigeria, Kenya na Afrika Kusini wanatarajiwa kupamba shughuli ya kuanza kwa msimu mpya wa show kabambe ya Big Brother Africa siku ya Jumapili tarehe 26 May.Show ya msimu huu imepewa jina la The Chase. Jumla ya washiriki 28 ambao wamechaguliwa kushiriki show ya mwaka huu watatambulishwa rasmi siku hiyo katika tukio ambalo linatarajiwa kuonyeshwa “Live” katika nchi zizizopungua 50.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari, tukio hilo litaanza kuonyeshwa saa moja jioni kwa saa za Afrika ya Kati (19:00 CAT) katika AfricaMagic, AfricaMagic Entertainment, AfricaMagic World na pia kwenye channel 197 na 198 katika DStv.
Msanii kutoka nchini Kenya,STL anayetamba na vibao vyake kama vile “Take My Time” , “Hula Hoop“, “Bad as I Wanna Be“, mshindi wa tuzo za Kisima, Clops na Jeermaan ameahidi kuzikonga vilivyo nyoyo za mashabiki wa muziki na hususani mashabiki wa Big Brother Africa.
Taarifa hiyo inazidi kupasha kwamba kutoka nchini Nigeria, wasanii Don Jazzy, D’ Prince n’ Wande Coal wanatarajiwa kuwakamata vilivyo mashabiki. Don Jazzy, mshindi wa tuzo mbalimbali kama prodyuza, mwimbaji na mwandishi na mwanamuziki atakuwa bega kwa bega D’ Prince na Wande Coal wakitumbuiza na vibao vyao kama vile “I like What I See”, “Bumper 2 Bumper” na “Who Born the Maga”.
Kisha kundi maarufu la muziki wa Afro Pop kutoka Afrika Kusini la Mafikizolo linatarajiwa kuwa kivutio cha kipekee wakati za uzinduzi huo. Kundi hilo ambalo mpaka sasa limeshaweka kibindoni tuzo mbalimbali linatarajiwa kuteka mashabiki kwa nyimbo zao kama vile ”Sibongile”, “Ndihamba Nawe”, “Nisixoshelani” na “Khona”.
Ni muda kidogo hatujasikia kitu kutoka kwa Abby Skills ambaye kwa watu wanaokumbuka enzi zile Bongo Fleva inaanza kushika kasi, mtamkumbuka vizuri. Huu hapa ni wimbo wake mpya akiwa amemshirikisha Chege. Wimbo unaitwa Shanni na Jenny. Msikilize
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Pichani Professor Jay akiwa na Kiboya,mdau mkubwa wa muziki nchini ambaye pia ni mwanachama wa CHADEMA. Picha kwa hisani ya Twitter ya Professor.
Habari ambazo zinatambaa hivi sasa mtandaoni ni kwamba msanii maarufu na miongoni mwa wanaoaminika kuwa waasisi wa muziki wa Hip Hop nchini Tanzania, Professor Jay (jina halisi Joseph Haule), amejiunga rasmi na harakati za siasa nchini kwa kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Professor Jay ambaye tungo zake mara kwa mara zimekuwa zikijikita katika kutetea maslahi ya wananchi, amejiunga na CHADEMA huko Dodoma ambapo amekabidhiwa rasmi kadi ya uanachama.
Zoezi hilo limesimamiwa na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo na Joseph Mbilinyi (Sugu) Mbunge wa Mbeya Mjini na kushuhudiwa na wanachama wengine kadhaa ambao aidha ni wanamuziki pia au wadau wa karibu wa muziki.
Bila shaka kujiunga kwa Professor Jay na CHADEMA kunaashiria kwamba yupo mbioni kugombea Ubunge katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. Professor Jay ni mwenyeji wa Mikumi-Morogoro na hivyo haitoshangaza kama ataamua kugombea katika jimbo hilo hapo mwaka 2015.
Professor Jay akikabidhiwa kadi na Mh.Joseph Mbilinyi.




sending...



















