Kila mtu, katika wakati fulani maishani mwake, huweza kuwa anafanya kazi ambayo kimsingi haipendi. Kama leo hii unaipenda kazi yako kiasi kwamba ukisikia jogoo la asubuhi linawika kuashiria kwamba kumekucha na  muda wa kazi umefika unafurahia na kutoa tabasamu zito,basi una bahati.Kwa upande mwingine yawezekana wewe upo katika lile kundi la watu ambao siku mpya ni siku mbaya.Ukiwaza juu ya kazi yako ghafla unapandwa na hasira. Unatamani usiende kabisa kazini.

Yawezekana ni kwa sababu masaa ya kazi yako ni mabaya.Unajihisi kama mtumwa.Mshahara ni mdogo sana na haukidhi kitu.Yawezekana huipendi kazi yako kwa sababu ya wafanyakazi wenzako ambao kutwa ni umbea tu na kukusemasema.Kwa kifupi wanakuudhi.Au yawezekana hupatani hata kidogo na bosi wako. Kwa ufupi ni kwamba kazi zinazochukiwa au watu wanaochukia kazi zao ni ukweli mtupu katika maisha yetu ya sasa.

Pamoja na kwamba unaichukia kazi yako na unatamani kuiakacha tangu majuzi, yapo mambo ambayo unaweza kuyafanya ili kukabiliana nayo na kupata kile unachokitaka na kuwa na furaha yako japokuwa huipendi kazi yako,huyapendi mazingira ya kazi yako nk;

Tambua Kwanini Upo Hapo

Sababu mbalimbali huchangia katika maamuzi ya kuanza kufanya kazi katika sehemu fulani.Yawezekana mwanzoni ulipenda mazingira ya kazi yako.Yawezekana ulihitaji kupata kazi ili uweze kujitoa katika hali duni uliyokuwa nayo.Ulihitaji kazi ili kulipa madeni yako,ili kulisha familia yako.Ipo sababu.

Ukiweza kukumbuka sababu ya msingi au ya mwanzo iliyofanya ukakubali kufanya kazi unayofanya,hiyo itakusaidia kubakia na akili timamu unapokuwa hapo ulipo.Jitahidi kukumbuka yote yaliyojiri wakati unatafuta kazi hiyo.Kumbuka jinsi ulivyohangaika kuandika barua za maombi,kumbuka usaili ulivyokwenda,uliyoyasema na kuahidi.

Kumbuka ulivyoongea na wenzako kuhusu kazi yako,ulipopata kazi nk Mambo yote haya yatakukumbusha kwamba wewe ni zaidi ya kazi yako.Kwamba uliichagua au kuikubali kazi uliyonayo kwa sababu nzuri tu.Kama sababu iliyokufanya uchague kazi hiyo hapo mwanzo haipo tena,basi upo ulazima wa kuiangalia upya kazi yako. Kumbuka kwamba unaweza kufanya hivyo kwa sababu wewe ni zaidi ya hiyo kazi uliyonayo na sio vinginevyo.Tabasamu tu,endelea na kazi huku ukiwa umefungua akili zote.

read more

John Shibuda, Mbunge wa Maswa Magharibi (CHADEMA). Soma Hapa kuhusu kinachomfanya apambe kurasa za mbele za vyombo vya habari.

Mchezaji mahiri wa Timu ya Simba ya Dar-es-salaam na Timu ya Taifa Ya Rwanda(Amavubi),Patrick Mafisango (32) hatunaye tena.Patrick Mafisango amefariki dunia alfajiri ya  leo jijini Dar-es-salaam kwa ajali mbaya ya gari iliyotokea maeneo ya Chang’ombe Veta.Marehemu alikuwa njiani kuelekea nyumbani kwake akitokea Maisha Club-Oysterbay.

Mipango ya kuusafirisha mwili wa Marehemu kwenda kwao nchini Rwanda inafanywa na uongozi wa Simba kwa kushirikiana na Ubalozi wa Rwanda Tanzania. Patrick alikuwa ameteuliwa kuwemo katika kikosi cha Rwanda kinachotarajiwa kuingia kambini Ijumaa hii kwa ajili ya kuikabili Algeria katika kuwania nafasi ya kucheza katika Fainali za Kombe la Dunia 2014 zinazotarajiwa kufanyikia huko Brazil.

Patrick Mafisango alizaliwa nchini DR Congo tarehe 7 March mwaka 1980 ambapo aliwahi pia kuchezea timu ya TP Mazembe kabla ya kujiunga na APR ya Rwanda na kisha ATRACO FC ya Rwanda na  baadae Azam FC ya Tanzania kabla ya kutua Simba Sports Club.

BC inapenda kuungana na wapenzi wote wa soka nchini,hususani wale wa Simba katika msiba huu mzito na pia kutoa pole nyingi kwa ndugu jamaa na marafiki wa Patrick Mafisango.Amina.

Hii hapa chini ni Taarifa ya Tanzania Football Federation ya Kuomboleza msiba huo

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mchezaji wa Simba na timu ya Taifa ya Rwanda (Amavubi), Patrick Mafisango kilichotokea leo alfajiri (Mei 17 mwaka huu) kwa ajali ya gari Dar es Salaam.

Msiba huo ni mkubwa kwa familia ya mpira wa miguu kwani Mafisango kwa kipindi chote alichocheza mpira hapa nchini akiwa na timu za Azam na baadaye Simba, aliifanya kazi yake (kucheza mpira) kwa bidii.

Kifo chake ni pigo kubwa si tu kwa familia yake na timu alizochezea, bali ukanda mzima wa Afrika Mashariki na Kati ambapo changamoto zake zilikuwa dhahiri uwanjani.

Wakati mauti inamkuta, Mafisango alikuwa ameitwa Amavubi kwa ajili ya mechi za mchujo za Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika zinazochezwa mapema mwezi ujao.

TFF inatoa pole kwa familia ya Mafisango, klabu ya Simba, Shirikisho la Mpira wa Miguu Rwanda (FERWAFA) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

Mungu aiweke roho ya marehemu Mafisango mahali pema peponi. Amina

 

Unaweza ukajiuliza sana kwanini Q-Chief alikuwa kwa muda mrefu kidogo ametulia kabla ya kuanza kuachia “mabomu” takribani tangu mwaka jana hivi.Nasema unaweza ukajiuliza kwa sababu kwa mapana Q anaweza.Ana kipaji na pengine kama alivyowahi kuniambia katika mahojiano baina yangu naye miaka ya nyuma kidogo, yeye ni tajiri wa sauti.

Lakini pengine tusijiulize sana.Si tushawahi kusikia habari za kimya kingi kina mshindo mkuu?Huenda.Au wewe unasemaje?Husikii?

Hapa ni wimbo mpya kutoka kwa Q-Chief ambaye pia anajulikana kama Q-Chilla achilia mbali majina mengine aliyojipachika mwenyewe kama vile Savimbi nk.Wimbo unaitwa Ungeniumiza. Can you relate to this song?Ukachungulia mbele ya safari ukaona kiza kitupu.Unapotoka ni karibu kuliko unapokwenda.Ukaona isiwe tabu,ngoja niishie hapa.Ni mapenzi yenye upofu na kisha kama vile Mwana wa Yule Mnazareti alivyokuwa akigusa watu wakaona tena,na wewe huyooo,ghafla unaona tena.Maisha.Msikilize Q-Chief hapa

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

Mwasiti is for sure one of the songbirds from Tanzania. She hails from the roots of Tanzania House of Talents(THT) which in my opinion, is a great place for youngsters who have got talents but have no good direction on how to develop them.

The name of the song is Nipishe-Mapito.It is a collabo but the sender didn’t mention the second partner and we decided to take it that way for now.Listen

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

 

Warembo watakaoziwakilisha Nchi zao katika mashindano ya Miss East Africa mwaka huu wanaendelea  kupatikana kutoka katika Nchi mbalimbali zinazoshiriki mashindano hayo.

 

Mrembo mwingine aliyeingia fainali ni Miss Lula Teklehaimanot (19) kutoka Nchini Ethiopia ambae alipatikana mwishoni mwa wiki baada  ya kuwashinda warembo wenzake waliojitokeza kutaka kuiwakilisha Ethiopia katika fainali hizo.

 

Miss Lula Teklehaimanot ana urefu wa 1.79m  na uzito wa 52kg ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika chuo cha St. Merry University cha jijini Addis Ababa, Ethiopia ampapo anasomea degree ya Marketing

 

Pia Mrembo huyo ni miongoni mwa wanamitindo maarufu  wanaochipukia kwa kasi Nchini Ethiopia.

 

Fainali za mashindano ya Miss East Africa 2012 zitafanjika tarehe 07 mwezi September mwaka huu jijini Dar es salaam ambapo zitashirikisha Nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia, Djibouti, Eritrea, Sudan, Ethiopia, Malawi, Madagascar, Reunion, Comoros, Seychelles, na Mauritius.

 

Mashindano ya Miss East Africa yanaandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Ltd ya jijini Dar es salaam

It has been a while since we heard something new from Pipi. Well..better late than never. Here is the new one from Pipi produced by Pancho Latino.The name of the track is Unapokuwa Mbali which can be literally translated into When You Are Far.Listen

Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

 

Yapo mambo ambayo hata unapotaka kuyakalia kimya tu inakuwa shida kidogo.Jana,Shirika La Ndege Tanzania(ATC) limepata ndege mbadala(nasema mbadala badala ya mpya kwa makusudi).Ndege hii imekodishwa.Uwezo wa kununua bado hatuna.Ukikodisha kitu maana yake kiasi fulani cha iliyokuwa iwe faida yako,inakwenda kwingine. Kimsingi tunakuwa tumejikomboa kidogo sana.

Pamoja na hayo,kwetu sisi yaelekea kuwa na ndege ya kukodisha ni mafanikio makubwa sana.Yanastahili makofi,vigelegele na keki.Kweli??

Wafanyakazi wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) wakishuka katika ndegempya aina ya Boeing 737-500 iliyokodishwa na shirika hilo yenye uwezo wa kubeba abiria 108. Ndege hiyo itaanza kuruka baada ya wiki moja.

Kaimu Mkurugenzi na Mwenyekiti Mtendaji wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) Paul Chizi akiongea na waandishi wa habari mara bada ya kuwasili kwa ndege mpya aina ya Boeing 737-500 iliyokodishwa na shirika hilo yenye uwezo wa kubeba abiria 108.

Wafanyakazi wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) wakikata keki kusherekea ujio wa ndege ndege mpya aina ya Boeing 737-500. Wapili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi na Mwenyekiti Mtendaji wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL ) Paul Chizi

Picha na maelezo ya picha kwa hisani ya G.Sengo

 

Katika lugha ya Kiingereza neno rahisi sana la kumuelezea Mtangazaji Ephraim Kibonde ni “Controversial“. Mara kadhaa ameingia katika mazungumzo ya wananchi kwa sababu tofauti tofauti.Lakini kubwa ni kwa sababu yeye hupenda kusema vile anavyofikiria.Haogopi.Kama anakuwa ametumwa au ni fikra zake mwenyewe,hilo ni jambo ambalo kila mtu,mimi na hata wewe,yambidi kuamua mwenyewe.

Yeye ni MC wa siku nyingi sana.Ana uzoefu mkubwa.Iwe ni send off,kipaimara,ubatizo,mkutano wa kimataifa,wa Chama nk Ephraim atauendesha vyema.Lakini mbali na shughuli za “usheherekeshaji”,Ephraim ni miongoni mwa watangazaji wanaoendesha kipindi cha Jahazi kinachorushwa na Clouds FM.Na hapo ndipo anapopata uhuru zaidi wa kuwafikia watu wengi.Na hapo ndipo neno “Controversial” linapokuja.

Jumatatu iliyopita,ilikuwa ni zamu yake katika Mkasi.Mtazame,msikilize hapa chini akiongea na Salama Jabir

You need to a flashplayer enabled browser to view this YouTube video

Warembo watakaoziwakilisha Nchi zao katika mashindano ya Miss East Africa mwaka huu wameanza kutangazwa.
Mrembo wa kwanza kupatikana ni Miss Rahwa Afework (22) kutoka Nchini Eritrea ambaye aliwashinda wenzake waliojitokeza kutaka kuiwakilisha Eritrea katika mashindano hayo.
Miss Rahwa Afework mwenye urefu wa 1.73m anasomea mambo ya Fashion design Nchini Eritrea.
Habari na picha kwa hisani ya Super D
Fainali za mashindano ya Miss East Africa 2012 zitafanjika tarehe 07 mwezi September mwaka huu jijini Dar es salaam ambapo zitashirikisha Nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia, Djibouti, Eritrea, Sudan, Ethiopia, Malawi, Madagascar, Reunion, Comoros, Seychelles, na Mauritius.
Mashindano ya Miss East Africa yanaandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Ltd ya jijini Dar es salaam

Read the Next Page →

↑ Go Back to Top of Page