BONGO CELEBRITY

All You Wanted To Know But Didn’t Know How and Where

MPIGIE KURA AMANDA OLE SULULU July, 4, 2008

Filed under: Fashion, Sanaa/Maonyesho, Urembo, Watu na Matukio — bongocelebrity @ 3:01 pm

Shindano maarufu la kumtafuta Miss Universe 2008 limeshaanza kupamba moto.Kilele cha shindano hilo ni tarehe 13 Julai 2008 huko jijini Nha Trang nchini Vietnam.

Mrembo anayeiwakilisha Tanzania ni Amanda Ole Sululu(pichani akiwa amevalia vazi la kiasili/kitaifa).Sasa kama mjuavyo,Miss Universe huendana na kupigiana kura.Unachoombwa ni kumpigia kura Amanda Ole Sululu ili ashinde kipengele cha Vazi la Taifa.Upigaji kura unaanza Jumatatu 7,Julai. Tembelea ukurasa wa kupigia kura kwa kubonyeza hapa.Hima watanzania.Kila la kheri Amanda.

 

HASIRA SIKU ZOTE NI HASARA? July, 4, 2008

Filed under: Burudani, Muziki, Weekend Special, Zilipendwa — bongocelebrity @ 12:05 am

Ni wiki nyingine tena, ni mwisho mwingine wa wiki.Mwaka 2008 unazidi kuyoyoma.Kwa wengi waliopo ‘ughaibuni” ni majira maarufu ya summer.Hapo ni mwendo wa watu kujianika juani kama vile hawajawahi kuona jua.Kwa wengi summer ndio maisha,ndio raha ya kuwepo duniani.Ni mwendo wa bikini na vilazia vyenye kuonyesha maungo yote.Majaribu.

Kwetu sisi wengine,kila siku ni summer.Hiyo ndio bahati tuliyojaliwa na Mwenyezi Mungu.Kwetu jua halikomi.Fukwe nzuri nzuri tunazo.Tushindwe wenyewe tu.Au sio?

Kama ilivyo ada,hapa kwetu mwisho wa wiki ni muda wa kukumbushana kulee tulikotoka.Wengi tunasema enzi zile zilikuwa nzuri kuliko enzi hizi.Kuna wengine wanakataa.Wanasema hivi sasa ndio mambo yote.Kuna mitandao,kuna ipod,maendeleo makubwa ya sayansi na tekinolojia.Wanasema dunia yao ni kama kijiji haswa.Wa zamani nao wamesimama waliposimama.Wanasema kwanza wao ndio wameandaa mazingira haya ya leo kwa hiyo vijana wa leo wasijitape kupita kiasi.Basi tu ni mijadala kila siku.Tena mirefu isiyo na hata dalili ya kikomo.Sijui wewe unasemaje.

Ngoja nikatize maneno mengi.Leo tunao tena “Nginde” yaani si wengine bali Mlimani Park Orchestra.Wimbo unaitwa Hasira.Je ishawahi kukutokea ukamuacha mama watoto wako au la azizi wako wa karibu kutokana tu na hasira halafu baadaye ukajutia kitendo chako?Halafu huyoo ukaamua kwenda kuomba msamaha kabla hujakuta kumbe kuna gharama kubwa za kurudiana?Sikiliza wimbo Hasira hapo chini.Wikiendi njema.

 

OLD SCHOOL PARTY KURUSHWA “LIVE” KUPITIA BongoRadio July, 3, 2008

Filed under: Tangazo/Matangazo, Watu na Matukio, Weekend Special — bongocelebrity @ 9:32 pm

Natumaini mpaka hivi sasa utakuwa umeshasikia kwamba tarehe 5 Julai 2008(jumamosi) ndani ya jiji la Columbus huko katika jimbo la Ohio nchini Marekani,kutakuwa na party ambayo waandaaji wameiita Old School Party of The Century. Kama bado hujasikia kuhusu hiyo party,bonyeza hapa na hapa ili kupata habari hiyo.

Lakini kama umesikia kuhusu party hiyo lakini kutokana na sababu moja au mbili hutoweza kuhudhuria,habari njema ni kwamba bado utaweza kusikia matangazo ya moja kwa moja(live) kutoka ukumbini hapo.Bongo Radio,radio pekee ya kitanzania mtandaoni,ndio itarusha shughuli hiyo “live”.

Unachotakiwa kufanya ni kuingia katika www.bongoradio.com kuchagua player unayotaka kutumia na kisha utakuwa umejumuika na maelfu ya watanzania wanaotarajia kuhudhuria party hiyo.Kumbuka burudani ya siku hiyo itashushwa na Djs wakongwe na wazoefu kama vile Dj Luke( Mix Master),TNT Jackson na bila kumsahau Bonny Luv kutoka Bongo.Matangazo “live” yataanza kurushwa kuanzia saa tatu usiku(9:00pm) kwa saa za Columbus,Ohio.

Kwa habari zaidi bonyeza hapa

 

WAMJUA HUYU? July, 2, 2008

Filed under: Burudani, Sanaa/Maonyesho — bongocelebrity @ 8:29 pm

Photo/A.Mrisho

 

ISSA MICHUZI NA HATUA MBILI MBELE July, 2, 2008

Filed under: Blogs, Mtandao, News, Sayansi na Tekinolojia, Tangazo/Matangazo — bongocelebrity @ 10:17 am

Kuanzia usiku wa leo(saa sita usiku kwa saa za Afrika Mashariki),blog maarufu ya Muhidin Issa Michuzi,itabadilisha anuani.Badala ya kupatikana kupitia www.issamichuzi.blogspot.com sasa itapatikana kupitia www.michuzi-blog.com.

Mbali na mabadiliko hayo ya anuani,yupo “mwana” mwingine ambaye naye anazaliwa.Hiyo ni tovuti nyingine chini ya usimamizi wa huyu huyu gwiji wa blog. Tovuti hiyo ambayo inapatikana kupitia www.bongotyube.com ni maalumu kwa habari,burudani,michezo nk kupitia video.

Kama kawaida yetu,tulipopata habari kuhusiana na mabadiliko hayo katika blog hiyo ya jamii pamoja na tovuti mpya inayoanzishwa,tuliona ni heri tumtafute Michuzi mwenyewe ili atupe undani kidogo kuhusu mabadiliko hayo nk.Kwa uungwana kabisa akakubali kufanya nasi mahojiano utakayoyasoma hivi punde ingawa ukweli ni kwamba yuko bize ili kuhakikisha kwamba mabadiliko yaliyotajwa hapo juu yanakwenda salama kabisa.

Lakini pamoja na kuongelea mabadiliko hayo,Issa Michuzi,ametoa mafunzo na changamoto muhimu sana kwa wanablog na pia washika dau mbalimbali katika sekta au fani ya habari na mawasiliano.Je ni changamoto na mafunzo gani?Anawaambia nini “wadau” wakati huu anapojiandaa kuendeleza “libeneke” kwa mapana na marefu zaidi? Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo;

(more…)

 

MISS TANZANIA EU 2008 NI LUCY FUNDIKIRA July, 1, 2008

Filed under: Bongo Flava, Urembo, Watanzania Kimataifa — bongocelebrity @ 1:36 pm

Pichani ni binti aitwaye Lucy Mwiza Fundikira ambaye hivi majuzi amejinyakulia taji la Miss Tanzania 2008 EU (nchi za Schengen).Shindano hilo lililofanyikia katika mji wa Essen nchini Ujerumani,lilipambwa pia na mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya,Ali Kiba(kama inavyoonekana katika picha hapo chini) ambaye yupo ziarani katika nchi mbalimbali za Ulaya.

Lucy Fundikira ana umri wa miaka 18 na anaishi na wazazi wake katika mji wa Rotterdam nchini Uholanzi.Kwa picha na habari zaidi kuhusu tukio hilo bonyeza hapa.

Ali mwana wa Kiba akiwarusha mashabiki huko Essen,Germany.

 

UJUMBE KUTOKA KWA WADHAMINI July, 1, 2008

Filed under: Safari, Tangazo/Matangazo, Wadhamini/Sponsors — bongocelebrity @ 12:02 pm

Kwa habari zaidi bonyeza hapa.

 

MwanaFA UNAOA LINI…? June, 30, 2008

Filed under: Bongo Flava, Burudani, Muziki, Single/Mpya — bongocelebrity @ 9:37 pm

Kwa mila na taratibu za jamii nyingi,hususani zetu za kiafrika,kijana akifikia umri fulani huwa anategemewa kuoa.Ikitokea ukafikia umri ambao kila mwanajamii anakutegemea “kujipatia jiko” na ukawa hujafanya hivyo, hapo lazima ujiandae na swali;unaoa lini?Ukikutana na shangazi swali ni hilo hilo.Ukikutana na mjomba naye anasimamia hilo hilo.Jamii nzima inauliza,unaoa lini?

Sasa je ukiulizwa swali hilo huwa unajibu nini?Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya,Hamis Mwinjuma a.k.a MwanaFA a.k.a Binamu anakupa msaada wa majibu katika single yako mpya inayokwenda kwa jina Bado Nipo Nipo huku akiwa amemshirikisha Miss Universe Tanzania 2007,Flaviana Matata.

Bado Nipo Nipo imepikwa na producer Harmy B.Pia MwanaFA anapewa tough na vichwa vingine kama vile Ambwene Yesaya(AY),Alan,Jabiri,Shehe na mwanadada aitwaye Anna.

Usikilize wimbo Bado Nipo Nipo kwa kubonyeza player hapo chini.Ningependa sana kusikia majibu kutoka kwa kinadada walio single, ni kweli anayoyasema MwanaFA?

 

KUTOKA MISRI NA MUSTAKABALI WA ZIMBABWE June, 30, 2008

Filed under: News, Serikali/Uongozi, Siasa — bongocelebrity @ 8:49 pm

Mkutano wa 11 wa Umoja wa Afria (AU) umeanza huko nchini Misri katika mji maarufu kwa utalii wa Sharm El Sheikh. Suala la Zimbabwe ndilo linaelekea kuugubika mkutano huo.Dunia nzima inasubiri kusikia kitakachoamuliwa au kuafikiwa huko Misri.

Rais wa Tanzania na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU),Jakaya Mrisho Kikwete,akifungua rasmi mkutano wa 11 wa nchi wanachama wa umoja huo huko Sharm El Sheikh nchini Misri jana.

Kutoka kushoto kwenda kulia ni Rais wa Tanzania na pia Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, Jakaya Mrisho Kikwete, Mwenyeji wa mkutano huo,Rais wa Misri Hosni Mubarak na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,Dr.Asha Rose Migiro.

Picha zote/Freddy Maro

 

MUGABE:KIELELEZO CHA UONGOZI AFRIKA? June, 30, 2008

Filed under: Editorial, Mawazo/Tafakuri, Serikali/Uongozi, Siasa, Special Interest News — bongocelebrity @ 6:29 pm

Katika anga za siasa duniani hivi leo,lipo jina ambalo dunia nzima inaendelea kulizungumzia.Hilo si lingine bali lile la Rais wa Zimbabwe, Robert Gabriel Mugabe.Kwa wengine mtu huyu ni shujaa,kwa wengine mtu huyu ni kinyume kabisa cha neno shujaa.Kwako wewe je?Je viongozi wa Afrika wanaohudhuria kikao cha Umoja wa Afrika huko Misri(na Mugabe naye anahudhuria) wataweza kumnyoshea vidole Mugabe?Nini hatma ya siasa za Afrika?

Pichani ni Rais Mugabe akiwa na mkewe,Grace Mugabe.Wengi wanasema wakati wao wanatafuna keki,wananchi wengi wa Zimbabwe wanakufa njaa.

Photo/New York Times