
Muimbaji wa nyimbo za Injili(Gospel) Upendo Nkone (pichani) anatarajiwa kufunga ndoa tarehe 17 October 2010 na Mchungaji John Mbeyela ambaye pia ni mjane mwenye watoto watatu.Ndoa hiyo itafungwa katika kanisa la Naioth kwa Mchungaji Mwasota.
Kwa mujibu wa mtandao wa Strictly Gospel,ndoa hiyo inakuja baada ya miaka 9 ya kuwa mjane. Upendo Nkone tayari anazo albamu tatu kibindoni zikiwa ni Mungu Baba,Hapa Nilipo na Zipo Faida.
We wish them all the best.
Photo Courtesy of Waimbaji wa Muziki wa Injili Tanzania Photostream
Ijumaa imewadia.Kama kawaida hii ni siku ambayo watu wengi,hususani wanaofanya kazi ya Jumatatu hadi Ijumaa,huwa wanaisubiri kwa hamu. Hapo sijasema kwamba wikiendi hii ni “Mwisho wa Mwezi”.Kila mtu anazo.Bahati nzuri ni kwamba bado tupo katika Mwezi wa Toba kwa hiyo vibweka huko mitaani navyo huwa vinapungua. La sivyo,ungesikia vibweka kutoka katika baa ya kona.Sikia vicheko.Sikia jinsi baa medi anavyokaripiwa akichelewa kuweka bia mezani.Jeuri ipo.Pesa huwa inaongea.
Nasi hapa BC,tupo kwa ajili ya kuendeleza jadi.Ijumaa ni siku ya kujifaragua kidogo.Zamani walikuwa wanasema siku ya “kuruka majoka”.Ni wakati wa Zilipendwa. Leo tungependa kukuhamisha kidogo msomaji na mpenzi wa safu hii ya kila Ijumaa.Hatukupeleki mbali sana.Ni hapo DRC.Zamani iliitwa Zaire.Ilikuwa maarufu sana ulimwenguni hususani baada ya ule mpambano wa ndondi za uzito wa juu baina ya Mohamed Ali na George Foreman mwaka 1974. Enzi za Mobutu Seseseko Nkuku wa Zabanga.
Wimbo unaitwa Mamou(Tu Vois?) kutoka kwa gwiji la magwiji katika Afro-Rumba.Si mwingine bali mzee mzima Francois Luambo Makiadi maarufu kama Franco.Wimbo huu ni hadithi tamu sana.Hadithi ya mapenzi,uongo katika mapenzi,maisha nk. Zamani nakumbuka tulikuwa tukitaniana kwamba wimbo huu na mwingine hivi wa Madilu System,ulikuwa ukiuanza basi unasafiri kutoka Dar-es-salaam mpaka Morogoro na bado unaburudika tu.
Naamini wimbo huu unaweza kukukumbusha mbali.Usiwe mchoyo basi wa kuwaambia wenzako kupitia sehemu ya maoni kwamba Mamou inakukumbusha wapi.Ulikuwa unasakata Rhumba sehemu gani? Nakutakia wikiendi njema.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Ukitaka kusoma tafsiri ya Kiingereza ya wimbo huu bonyeza hapa.

Sijui kama nitakuwa nimekosea nikisema kwamba pengine AY na MwanaFA mpaka hivi sasa wanaweza kuwa wanashikilia rekodi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao wameshirikiana zaidi katika kazi zao.Kumbuka hawa wametoka mbali tangu enzi zao wakiwa East Coast Team iliyokuwa ikiongozwa na King Crazy GK ambaye sina uhakika yuko wapi siku hizi na anafanya shughuli gani.
Kuthibitisha kuzidi kukomaa kwa ushirikiano wao,AY na MwanaFA wakimshirikisha Hard Mad,wameachia single inayokwenda kwa jina Dakika Moja. Hii ni production kutoka B’Hitz Production iliyo chini ya Hermy B.
Sikiliza hapo chini;Ujumbe ni kwamba anaomba dakika moja tu aseme yaliyopo moyoni.Mmh,inawezekana kweli ndani ya dakika moja kikaeleweka?Sijui.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.

SIKU 10 za mwanzo za kampeni za urais zilizoanza rasmi, Agosti 21, zimechukua mwelekeo wa malumbano na mvutano mkubwa wa hoja kati ya vyama viwili vya siasa; Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kile cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumatano umebaini kuwa malumbano hayo kwa kiwango kikubwa kiini chake ni kile kinachoonekana kuwa ni kuwapo kwa dalili za kuzidi kuimarika kwa ushindani mkali wa majukwaani kati ya wagombea wawili wa urais wa vyama hivyo, Rais Jakaya Kikwete (CCM) na Dk. Willibrod Slaa (CHADEMA).

Here is the official video for R.Kelly’s “When A Woman Loves” from his upcoming Love Letters EP to be released soon.When a woman loves…she loves for real.His words,not mine.

Former Big Brother Africa housemates(BBA4),Kevin Chuwang Pam(from Nigeria) and Elizabeth Gupta(from Tanzania) who recently announced their engagement, are now about to move into the really thing;marriage.
According to a source close to the couple, they are planning to tie the knot this coming December in Nigeria.Kevin is expected to visit Tanzania sometimes soon to meet Elizabeth’s family and adhere some customs and traditions before the big day.
Kevin was the winner of BB4 and many Tanzanians still remember how he embraced the Tanzanian flag when he was declared a winner.

Kuna kitu nimekipenda katika kuitazama kwa makini picha hii.Bahati mbaya siwezi hata kuelezea vizuri ni kitu gani nilichokipenda katika picha hii ya wanachama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) walipokuwa wakimshangilia mgombea Urais kwa tiketi ya chama hicho,Dr.Wilbrod Slaa,wakati wa ufunguzi wa kampeni za chama hicho katika viwanja vya Jangwani jijini Dar-es-salaam.
Ni matumaini, ni saa ya ukombozi,ni kwamba tumechoka sasa au?
Picha kwa hisani ya John Bukuku.
“Kama maisha tumejaliwa,kama vipaji tumeshapewa,kwanini leo tuogope?Wanafiki tuwashangae,Wanachekesha”
Si maneno yangu bali maneno kutoka kwa vijana wa TMK Majita.Yamo katika wimbo wao walioutoa hivi karibuni unaokwenda kwa jina la Wanachekesha.Hii ni production kutoka Sound Crafters Studio chini ya Producer Enrico na Muba Touch.Burudika.
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.



